Papa amewatakia Rais amani,ustawi na baraka ya Mungu Mwenyezi!
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Baba Mtakatifu ameingia uwanja wa ndege mida ya saa mbili asubuhi na kuondoka na ndege namba A320, inayojulikana "Aldo Palazzeschi. Aliyekuwa anawamsubiri Baba Mtakatifu katika Uwanja wa ndege Kimataifa Fiumicino ni viongozi wa serikali na dini, na kama kawaida ya tabasamu yake pamoja na mfuko wake mweusi mkononi mwake , amewasalimia kwa kupeana mkono na kuendelea kupanda ngazi hadi kufikia kilele cha ndege ambapo kabla ya kuingia amegeuka na kuwapungia wote walio kuwa wanamsindikiza kwa macho na furaha.
Baada ya kufika ndani ya ndege kama kawaida ameingia ndani na kuwasalimu hostess wawili na Rubani ambao walikuwa wanamsubiri. Baada ya kuwasalim hao amewageuka wengine na kuwapungukia mkono.
Kama desturi wakati wa safari yake kuelekea nchini Ireland ametuma Telegram kwa Rais wa Jamhuri ya nchi ya Italia , Bwana Sergio Mattarella. Katika Telegram ya Rais wa Italia imeandikwa: wakati ninaacha Roma kuelekea Ireland kwenye Fursa ya Mkutano wa Familia duniani, ninaombea taifa la Italia zawadi za kudumu, hekima kwa ajili ya kuendelea kuthamanisha na kulinda thamani ya ndoa na familia. Ninakutakia wewe na wahuduma wako heri katika shughuli za kuhudumia watu wa Italia ambao ninawatumia nao baraka.
Aidha Baba Mtakatifu pia ametuma telegram nyingine kwa Marais wa nchi zote anazopitia akiwa juu angani: Uswisi, Ufaransa na Uingereza ambapo amewatakia amani,ustawi na baraka ya Mungu Mwenyezi!