Tafuta

Kanisa halitakwenda mbele na Injili haitakwenda mbele kwa njia ya uinjilishaji usio na furaha, au wenye uchungu, vyote vitajikita mbele kwa njia ya furaha na ujazo wa maisha! Kanisa halitakwenda mbele na Injili haitakwenda mbele kwa njia ya uinjilishaji usio na furaha, au wenye uchungu, vyote vitajikita mbele kwa njia ya furaha na ujazo wa maisha! 

Papa Francisko:wakristo waoneshe furaha bila kufungwa na kasumba!

Msiwe na aibu kuonesha furaha ya kukutana na Bwana,msiwe mbali na watu wanapofanya siku kuu hasa wanapohisi ukaribu na Mungu.Ndiyo ushauri alioutoa katika mahubiri ya Papa Francisko kwenye Kanisa la Mtakatifu Marta,Vatican tarehe 28 Januari 2020. Papa anasema:Injili itakwenda mbele tu kwa njia ya uinjilishaji uliojaa furaha na maisha na furaha.Lakini ni faraha inayoendelea hata katikati ya meza ya familia pamoja.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Hisia za kuwa na furaha ya mkristo ndizo zimekuwa kipaumbele cha mahubiri Papa wakati wa Misa katika Kanisa la Mtakatifu Marta Vatican, Jumanne tarehe 28 Januari 2020. Ushauri huu umetokana na somo la kwanza la  Kitabu cha Pili cha Samueli mahali ambapo kuna simulizi ya Daudi na watu wote wa Israeli wakifanya shangwe kuu kutokana na  kurudishwa kwa  sanduku la Agano la Mungu huko Yerusalemu

Siku kuu ya watu ni kwa sababu Mungu yuko karibu

Sanduku lilikuwa limetekwa nyara, anaeleza Papa na sasa linaporudi ni shangwe kuu kwa watu hao. Watu walihisi kuwa Mungu yuko karibu na ndiyo maana wanafanya siku kuu. Wakiwa na Mfalme Daudi alifanya maandamano nao, wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana kwa kuwachinja ngómbe na kikono, watu walikuwa na cheleko, kelele, nyimbo na michezo.  Ilikuwa ni siku kuu, furaha ya watu wa Mungu kwa maana Mungu alikuwa nao Papa amesisitiza. Na Daudi? Papa anajibu kwama “Akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote kwa wote, alielezea furaha yake bila aibu; ni furaha ya kiroho ya kukutana na Bwana. Mungu amerudi kwao, hiyo inawapatia furaha kubwa.

Daudi alifanya shangwe kwakuwa alikuwa anampenda Bwana

Daudi hakufikiria kama yeye ni Mfalme na kama mfalme kwa kawaida alipaswa kuwa mbali na watu, yaani, ukuu wake na umbali… Lakini Daudi anampenda Bwana na kuwa na furaha ndiyo maana ya tukio hili la kupeleka sanduku la Bwana Papa Francisko amesisitiza. Tukio alilofanya Daudi linaelezea furaha hiyo, kwa kucheza na kuimba kwa hakika kama watu wote. Aidha Papa Francisko amebainisha kwamba tendo hilo ni kama lile  linatokea  hata kwetu kuhisi furaha hasa tunapokuwa na Bwana na labda katika parokia au katika nchi yoyote inapotokea sikukuu ya watu. Kadhalika ametaja  tukio jingine la historia ya Israeli walipopata kitabu cha Sheria, wakati wa enzi za  Nabii Neemia, hata wakati huo watu walilia kwa furaha na kufanya siku kuuu.

Kudharau ghafla dhidi ya  furaha

Maandishi  ya Nabii Samweli yanaendelea  kuelezea  jinsi ya kurudi kwa Daudi nyumbani kwake, ambapo alimkuta mmoja wa wake,  zake Mical, binti Sauli. Yeye alimkaribisha kwa dharau. Alipomuona mfalme akicheza, alimuonea aibu na kumkosoa akisema: Lakini je! hukuona aibu kwa kucheza kama mtu mchafu, kama mmoja wa watu?”. Kwa maana hiyo Papa Francisko anongeza:  “ hii ni dharau halisi  la kidini,  dharau la ghafla dhidi ya furaha na Bwana. Daudi alimweleza mwanamke  kwamba hii ilikuwa ni furaha ya ghafla kwa ajili ya Bwana. Ni furaha katika Bwana kwa kuwa tumerudisha Sanduku nyumbani! Lakini yeye aliendelea kudharau. Biblia inasema kuwa mwanamke huyo Mical, hakuweza kupata mtoto kwa tendo hili.  Bwana alimpatia adhabu. Unapokosa furaha ya kuwa mkristo Papa amesema, huwezi kuzaa matunda; unapokosa furaha ya moyo hakuna matunda.

Inahitaji uinjilishaji wa furaha ili kwenda mbele

Papa Francisko akiendelea na mahubiri yake amebainisha kuwa, furaha haijifafanui kwa njia ya kiroho tu,  bali inageuka ya kushirikishana. “Daudi siku hiyo baada ya kuwabariki akawagawia watu wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu. Basi watu wote wakaenda zao, kila mtu nyumbani kwake”. Na ili kila mmoja aweze kufanya sikukuu katika nyumba yake. Kwa maana hiyo Papa anasema: “ Neno la Mungu halionewi aibu katika siku kuu”. Ndiyo mara nyingine kuna hatari ya furaha kuzidisha  na  kuamini kuwa ndiyo kila kitu  lakini katika mantiki hii  kwa hakika ilikuwa ni hali ya furaha ya siku kuu. Hata Mtakatifu Paulo VI anakumbusha katika Wosia wake wa Kitume wa  “Evangelii Nuntiandi”, ambao anazungumzia mantiki hiyo na kushauri kuwa na furaha.

Kanisa na Injili vitajikita mbele ya safari kwa furaha na ujazo wa maisha

Kwa kuhitimisha Papa Francisko amesema: “Kanisa halitakwenda mbele na Injili haitakwenda mbele kwa njia ya uinjilishaji usio na furaha,  au wenye uchungu, hapana. Kanisa litakwenda mbele kwa njia ya uinjilishaji wa furaha na uliojaa maisha. Furaha katika kupokea Neno la Mungu, furaha ya kuwa mkristo, furaha ya kwenda mbele, kuwa na uwezo wa kufanya siku kuu bila aibu na siyo kuwa kama yule mwanamke Mical yaani kuwa Mkristo au Wakristo rasmi, wakristo wafungwa wa sheria na kasumba.

28 January 2020, 11:19
Soma yote >