Papa Francisko:Mungu ana uwezo wa kubadili yote.Tumshukuru wa neema zake!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Jangwa litachanua, amerudia rudia kusema Baba Mtakatifu Francisko wakati wa mahubiri yake kwenye misa ya asubuhi tarehe 19 Desemba 2019 katika Kikanisa cha Mtakatifu Marta mjini Vatican, huku akiangaziwa na masomo ya siku zaidi kwa Nabii Isaya. Na hiyo ni kutokana na Liturujia ya siku ambayo masomo yake yameonesha juu ya subir ana matumainia ya Siku kuu ya Kuzaliwa kwa Bwana na ni masomo ambayo yametuweka mbele ya majangwa mawili, yaani kuhusu wanawake wawili waliokuwa tasa kama Elisabeti mama yake Yoanhe Mbatizaji na mama yake Samsoni,amasema Baba Mtakatifu Francisko.
Bwana anafanya kuchanua maua katika jangwa
Ni Bwana anayefanya kuchanua maua katika jangwa amethibitisha Baba Mtakatifu. Wanawake wote wawili walipata mimba na kujifungua watoto. Kwa maana hiyo katika maswali hiyo si kwamba ni miujiza, bali huo ni msingi wake Mungu na ndiyo msingi wa imani yetu! Wanawake wawili waliweza kutunga mimba kwa sababu Mungu anao uwezo wa kubadili kila kitu hata sheria za asili; ana uwezo wa kutengeneza njia kwa kutumia Neno lake. Zawadi za Mungu ni za Bure. Maisha ya wanawake wawili hao, ni kielelezo cha zawadi ya bure ya Mungu, Baba Mtakatifu Francisko amebainisha.
Yote ni neema tu, kutoka kwa Mungu
Akitoa mfano kuhusu tabia za wale wanaodai kuwa ni wakatoliki kwa sababu wanakwenda kila Domika katika misa, au wanahusika katika chama chochote cha kiparokia Baba Mtakatifu Francisko ameuliza masawali kuwa, je hao wanafanya nini? Wananunua wokovu wao? Je wanaamini kwamba hayo yatawaokoa wanayofanya? Na kumbe, jibu ni kwamba utaokoka tu kwa sababu wewe unaamini kutoka zawadi za Mungu bure. Yote ni kwa neema tu! amesisitiza Baba Mtakatifu Francisko. Kwa kuhitimisha amesema kwamba, “ katika siku hizi kabla ya sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana, tumsifu Bwana kwa sababu ya zawadi yake ya bure ya wokovu, kwa ajili ya zawadi ya bure ya maisha na kwa ajili ya zawadi zote za bure anazotujalia. Yote ni kwa neema tu kutoka kwa Mungu!