Tafuta

Maandamamo kwa ajili ya heshima ya Mtakatifu Dominic wa Guzman huko Managua nchini Nicaragua Maandamamo kwa ajili ya heshima ya Mtakatifu Dominic wa Guzman huko Managua nchini Nicaragua  (ANSA)

Nicaragua,Gambera wa Seminari ya Matagalpa amewekwa gerezani

Padre Jarvin Tórrez,ambaye pia ni paroko wa Kanisa la Mtakatifu María wa Guadalupe,huko Matagalpa amewekwa gerezani tangu 5 Agosti.Hii iliripotiwa na wanaharakati na mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini ambapo ilifahamika pia kwamba Lesbia Rayo Balmaceda,mhudumu mlei wa parokia ya Sébaco,pia yuko kizuizini.

Vatican News

Padre mwingine alikamatwa Jumatatu tarehe 5 Agosti katika Jimbo Katoliki la  Matagalpa, nchini Nicaragua. Huyo ni Gambe wa Seminari Kuu yaya Falasafa ya  Mtakatifu Aloys Gonzaga na paroko wa Kanisa la Mtakatifu María de Guadalupe, katika kitongoji cha Guanuca cha Matagalpa. Kwa njia hiyo Padre Jarvin Tórrez, alipelekwa gerezani, kulingana na kile ambacho waamini waliambia vyombo vya habari. 

Kukamatwa kwa padre huyo kulishutumiwa na wanaharakati na mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini huo, yaliyonukuliwa na gazeti la kitaifa la “La prensa,” ambalo pia ilifahamika kuwa Lesbia Rayo Balmaceda, mhudhumu wa parokia ya Sébaco  Mlei pia yuko kizuizini.

Mapadre tayari  kumi na watatu wamefungwa katika muda wa Juma moja huko Nicaragua. Wao kwa kiasi kikubwa ni wa Jimbo la Matagalpa, ambapo Askofu wao, Rolando Álvarez, tayari alifukuzwa mbamo tarehe 14 Januari 2024. Mnamo Machi 2023, Jamhuri ya Nicaragua iliomba Vatican kufunga ofisi zao za kidiplomasia, bila kuvunjia kabisa uhusiano wao.

06 Agosti 2024, 17:13