Tafuta

Mama Maria: Mama Maria: 

Taasisi ya Kipapa ya Maria kuanzisha kituo cha uchunguzi wa mafumbo ya Maria

Lengo ni kuchambua na kutafsiri kesi mbalimbali za kuonekana,machozi,lakini pia maeneo ya ndani,unyanyapaa na matukio mengine duniani ambayo yanaendelea au tayari yametokea,lakini bado yanasubiri hukumu ya uhalisi na mamlaka ya kikanisa.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Ilianzishwa katika Taasisi ya Kipapa Kimataifa ya mafunzo ya (PAMI) Uchunguzi wa matukio na majabu ya mfumbo yanayohusiana na sura ya Bikira Maria ulimwenguni kwa lengo la kuchambua na kutafsiri matukio mbalimbali ya Mama Maria (Mariophanies) yaani kutokea, machozi, lakini pia maeneo ya ndani, kama vile unyanyapaa na matukio mengine ya fumbo ambayo yanaendelea au tayari yalitokea, lakini ambayo bado yanasubiriwa kutolewa tangazo kutoka kwa mamlaka ya kikanisa kuhusu uhalisi.

Msaada kwa masomo na usambazaji

Padre Stefano Cecchin(Ofm),rais wa Taasisi hiyo PAMI ameeleza kwamba lengo walilojiwekea ni kutoa msaada kamili kwa ajili ya utafiti, uthibitishaji na ufichuaji sahihi wa matukio hayo, ambayo siku zote huendana   na mafundisho  ya kikanisa, mamlaka husika na kanuni  kwa unaglizi wa  Vatican  juu ya mafundisho hayo. Mwangalizi atafanya kazi kwa utaratibu, kimkakati, taaluma mbalimbali na namna iliyohitimu, pia kwa ushirikiano na wataalam na watafiti, watu wa juu katika uwanja wa sayansi na mamlaka ya kikanisa. Ni muhimu kufafanua, kwa sababu ujumbe unaodaiwa mara nyingi huleta mkanganyiko, hueneza matukio ya siku ya mwisho yenye wasiwasi au hata shutuma dhidi ya Papa na Kanisa. Je, ni jinsi gani Mama Maria, Mama wa Kanisa, angeweza kudhoofisha uadilifu wake au kupanda hofu na upinzani, yeye ambaye ni Mama wa Huruma na Malkia wa Amani? Vivyo hivyo, ni muhimu kutoa msaada wa mafunzo kwa sababu kushughulikia kesi fulani kunahitaji maandalizi ya kutosha, alifafanua zaidi.

Tume za kitaifa na kimataifa

Kamati za kisayansi mahalia pia zitaundwa hivi karibuni, katika mantiki ya mtandao wa uendeshaji wenye uwezo wa kupanua wigo wa hatua. Mwangalizi  ambaye anaanza rasmi shughuli zake katika kikao cha kwanza  ambacho kitafanyika Jumamosi  tarehe 15 Aprili 2023 katika makao makuu ya  Tasisi hiyo PAMI Roma , mahali ambapo atafanyia kazi kwa kawaida, pia ataweza kukutana na kufanya kazi katika kambi hiyo  kulingana na mahitaji au maombi ya usaidizi.

Kukuza upyaisho na kujifunza matukio ya ajabu

Madhumuni ya uangalizi kwa mujibu wa maelezo ya rais ni kutenda kwa ufanisi na kwa njia nzuri ya  kuamsha tume za kitaifa na kimataifa za kutathmini na kujifunza matukio ya ajabu na matukio yaliyoripotiwa katika maeneo mbalimbali ya dunia, ili kukuza upyaisho  na mafunzo katika shughuli za aina hiyo ya matukio na maana zake nyingi za kiroho na kiutamaduni, ambazo zinakuza shughuli za kiwango cha juu za usambazaji na ushauri, hasa katika huduma ya Makanisa na Maaskofu wa mahali hapo, lakini pia shughuli za utafiti wa kinidhamu kwa kushirikiana na taasisi za kitaaluma, za walei na za kikanisa na uchapishaji wa matokeo ya tafiti zilizofanywa.

Uchunguzi wa matukio ya ajabu ya Maria katika Tassisi ya Kipapa ya kimataifa ya Maria
14 April 2023, 17:25