Tafuta

Ziara ya Papa Francisko nchini Sudan Kusini:Askofu Mkuu wa Addis Abeba:"nimeguswa sana na vijana wa Sudan kumwomba Papa awaombee". Ziara ya Papa Francisko nchini Sudan Kusini:Askofu Mkuu wa Addis Abeba:"nimeguswa sana na vijana wa Sudan kumwomba Papa awaombee". 

Kardinali wa Ethiopia:viongozi wa Sudan Kusini wasikilize sala ya Papa!

Askofu mkuu wa Addis Ababa, Kardinali Berhaneyesus Souraphiel,akiwa katika tukio la Papa Francisko mjini Juba alisema kuwa Bwana atasikia maombi na machozi ya watu.Vijana,ambao wamehama kwa miaka mingi,wanataka maisha ya kawaida,shule ya kawaida,wanataka kucheza na wamemwomba Papa awaombee:hii ilinigusa sana.

Na Angella Rwezaula; - Vatican.

Katika mahojiano na Vatican New, Kardinali Berhaneyesus Souraphiel wa Ethiopia, Askofu Mkuu wa Addis Ababa, akieleza kuhusu Ziara ya  Papa Francisko huko Juba, Sudan Kusini, alisema kuwa: "Wakati, Papa anazungumzia juu ya amani, upatanisho, msamaha na kuishi pamoja bila kuzingatia masilahi ya kikabila au mambo mengine, lakini kama watu wa nchi hiyo mpya, Sudan Kusini, nilisikia watu wakipongeza sana kwa makofi na nina matumaini kwamba viongozi hawa watasikiliza sauti'hiyo ya watu”. Ni matumaini ambayo Kardinali  huyo amekuwa nayo  wakati akishiriki katika matukio mbali mbali ya Baba Mtakatifu nchini Sudan ikiwa ni hatua ya pili ya Ziara ya 40 ya kitume, maba baada ya kutoka Cong DR iliyoanza tarehe 31 Januari na kuhitimishwa huko Sudan Kusini Dominka tarehe 5 Februari 2023.

Mkutano wa kiekuemene  wa Papa na viongozi wa Canterbury na Scotland
Mkutano wa kiekuemene wa Papa na viongozi wa Canterbury na Scotland

Akihojiwa na Vatican News kwa hiyo anashirikisha hisia na matakwa yake asa jambo ambalo lilimgusa na kwamba kwa ujumba tukio zima. Kwamba Papa alifika kama mtu rahisi na kwa urahisi huo pia alizindua wito huo, tena, kwa viongozi wa kiraia wa nchi hiyo mpya, Sudan Kusini. Wao walipata uhuru, na ambayo  ni nchi tajiri... Lakini je wamefanya nini? Hakuna cha zaidi ya migogoro na vita, vya wenyewe kwa wenyewe  ambavyo vimesababisha uharibifu mwingi, hasa uharibifu wa maisha. Watoto na vijana wengi wamekufa, akina mama na wazee wamekuwa wakimbizi, katika nchi zao na nje ya nchi.

Makambi ya wakimbizi wa ndani ya nchi
Makambi ya wakimbizi wa ndani ya nchi

Kuna mamilioni ya wakimbizi kwa sababu viongozi wa kiraia wanaweka  kwanza maslahi yao binafsi na madaraka. Papa Francisko kwa  miaka minne iliyopita aliwaalika jijini Vatican kufanya mafungo ya kiroho pamoja. Alibusu hata miguu yao akisema: “Mna wajibu wa kuwa karibu na watu wenu, si kuonesha uwezo, bali huduma, kama wachungaji wema”. Na hiyo ilienda vizuri sana lakini hali halisi bado ndani nchi.

Ziara ya Kitume nchini Sudan Kusini
Ziara ya Kitume nchini Sudan Kusini

Akielezea juu ya  uwepo wao mjini Juba kwa ziara ya Papa pia kwa  msaada kwa Baraza la Maaskofu wa Sudan Kusini alisema kwamba ni kweli Sudan na Sudan Kusini wana Baraza la Maaskofu sawa, na wako katika eneo linaloitwa Amecea, yaani Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu  wa kanda ya Afrika Mashariki, Afrika Kusini na Pembe ya Afrika. Kwa hiyo walikwenda kuwa  pamoja nao na kuwaonesha kwamba wako  pamoja wano na wanawaombe kwa sababu ziara hiyo ya kiekumene na ya amani ni maalum. Sio  kwa sababu tu ya uwepo wa Baba Mtakatifu Francisko, lakini pia kwa sababu Askofu Mkuu wa Canterbury na Msimamizi wa Kanisa la Scotland walkwenda huko. Watu hawa wote, jumuiya hizo, walikuwa kwenye uwanja wa ndege kuwapokea viongozi watatu wa kidini, ambao pia walisali kwa sala ya kiekumene ya Kikristo.

Vijana nchini Sudan Kusini wanatakiwa kuleta mapinduzi ya amani
Vijana nchini Sudan Kusini wanatakiwa kuleta mapinduzi ya amani

Kwa maana hiyo Kardinali alisema amavyo amni kwamba Bwana atawasikia, na watakatifu wote na wafia dini wote walioteseka hapo pia watasaidia. Yeye binafsi alisema anaomba kwamba watu wa Sudan Kusini wapate amani. Wengi wamefanyia kazi hilo, wamisionari wengi wametoa maisha yao kwa ajili ya hilo, na marafiki zao na majirani pia wameiombea nchi hiyo mpya. Na vile vile anaamini Bwana atasikia maombi hayo, na machozi, kwa sababu amesikia vijana, ambao wamehamishwa kwa miaka mingi. Wanataka kuwa na maisha ya kawaida, shule ya kawaida wanataka kucheza. Walizungumza na Papa juu ya haya yote na kuomba awaombea na hivyo kwa hakika lilimgusa sana. Hao waliomba  baraka kwa watoto wa Sudan Kusini na hiyo ilivutia sana.

Jamii bora inajengwa na wanawake kwa kushirikiana pamoja bila kumwacha yeyote nyuma
Jamii bora inajengwa na wanawake kwa kushirikiana pamoja bila kumwacha yeyote nyuma

 

07 February 2023, 12:48