Tafuta

Mgogoro nchini Ukraine Mgogoro nchini Ukraine 

Wasi wasi maaskofu wa Ulaya kwa ajili amani ya Ulaya na kwingineko!

Kwa mujibu wa Kardinali Hollerich,Rais wa Shirikisho la Mabaraza ya Umoja wa Ulaya katika taarifa yake inasema kwamba nguvu za kijeshi zinazovamia na kuendeleza vurugu na migogoro zinaweza kuharibu Ulaya kwa miaka mingi ijayo.Wanatoa wito kwa wakuu wa serikali ili waweze kuacha vita na kwa sababu vita daima ni kushindwa kwa ubinadamu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Katika taarifa zilizotolewa zenye wasiwasi wa maaskofu wa Umoja wa Ulaya kutokana na mivutano inayoendelea mipakani mwa Mashariki mwa Umoja wa Ulaya zinabainisha kuwa: “ uthibitisho na matendo ambayo sasa yanawakilisha tishio, ambalo si tu kwa ajili ya  Ukraine lakini pia kwa kuweka hatari hata ya amani ya bara zaima la Ulaya na kwingineko”.

Watoto wa shule wakiwa nje ya Madarasa wakati wa masomo wakifundishwa namna ya kujikinga na mabomu
Watoto wa shule wakiwa nje ya Madarasa wakati wa masomo wakifundishwa namna ya kujikinga na mabomu

Kwa mujibu wa Kardinali Jean-Claude Hollerich, Rais wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu ya Jumuiya za Umoja wa Ulaya katika taarifa iliyotolewa tarehe 26 Januari 2022 anasema kwamba nguvu za kijeshi zinazovamia na kuendeleza vurugu za migogoro  zinaweza kuharibu Ulaya kwa miaka mingi ijayo. Kama walivyo kuwa wamebainisha hata maaskofu wa Poland, kuhusiana na nguvu za uzoefu wa kizazi kilichopita, maaskofu hofu wanatoa wito kwa wakuu wa serikali ili waweze kuacha vita na kwa sababu vita daima ni kushindwa kwa ubinadamu.

Watoto wa shule wakiwa nje ya Madarasa wakati wa masomo wakifundishwa namna ya kujikinga na mabomu
Watoto wa shule wakiwa nje ya Madarasa wakati wa masomo wakifundishwa namna ya kujikinga na mabomu

Kwa kufanya kama mwangwi wa maneno ya Papa Francisko, Maaskofu wote wa Ulaya wanawaalika sehemu zote ili kuweka pembeni maslahi binafsi, kuacha kuhamasisha mizozo na badala yake  kuongeza imani kwa kutafuta wakati huo huo suluhisho la amani na kusaidia mgogoro unaoendelea ili mazungumzo ya wazi yaweze kuwapo yenye misingi ya haki kimataifa. Maaskofu aidha wanashauri jumuiya ya kimataifa pamoja na ya Umoja wa Ulaya, kupyaisha jitihada zao kwa ajili ya amani na kuchangia uhai wote katika  jitihada hizi za mazungumzo, bila kuonesha nguvu na kuongeza silaha, badala yake kutafuta njia za ubunifu wa kufanya michakato ya amani na jihudi zenye misingi ya thamani adili.  Hata hivyo Maaskofu Barani Ulaya  wanakaribisha tangazo la hivi karibuni la Tume ya Ulaya la kutoa kifurushi kipya cha usaidizi wa kifedha cha Euro bilioni 1.2 kwa ajili ya Ukraine na kutoa wito wa kupitishwa na kutekelezwa kwa haraka kwa manufaa ya watu wa Ukraine.

27 January 2022, 16:34