Tafuta

Mkutano Mkuu XX wa AMECEA unatarajiwa kufanyika Dar Es Salaam Tanzania. Mkutano Mkuu XX wa AMECEA unatarajiwa kufanyika Dar Es Salaam Tanzania. 

Mwezi Novemba AMECEA itazindua Mkutano wake mkuu wa XX

Bodi ya Utendaji ya shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Afrika Mashariki AMECEA,katika mkutano wao mnamo Oktoba 21,wameazimia kuwa Jumapili,tarehe 7 Novemba kuzindua Mkutano Mkuu ujao wa XX unaotarajiwa kufanyika mnamo 2022,katika nchi mwenyeji wa mkutano huo nchini Tanzania.

Na Sr. Angella Rwezaula – Vatican.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa AMECE, Padre Anthony Makunde wakati akihojiwa mnamo Ijumaa tarehe 22 Oktoba 2021 amethibitisha kuwa “Baada ya kutathimini hali halisi ya sasa ya UVIKO -19 katika kanda, tumeona kuwa inahitajika kuzindua Mkutano Mkuu wa 20  mwezi Novemba ili  kuanza maandalizi na kuona jinsi gani tutaweza kukabiliana na janga. Hata kama tunazamia kufanya mkutano kwa uwepo mwezi Julai ujao, bodi bado itatazama hali halisi ya janga kufikia mwishoni mwa mwezi Januari 2022 kwa kutathimini  uwezekano wa kuwa na mkutano huo au hapana na kwa maana hiyo maamuzi ya mwisho yatafanyika mwezi Februari”.

Kama mambo yatakwenda sawaJulai mkutano wa XX utafanyika Dar es Salaam

Katibu Mkuu wa AMECEA aidha alisema kwamba ikiwa kila kitu kitakwenda vizuri, mkutano huo utaweza kufanyika katika Juma la pili la mwezi Julai 2022, jijini  Dar es Salaam Tanzania, kwa ufunguliwa na Misa, siku ya  Jumapili tarehe 10 Julai 2022. Wakati wa mkutano wao uliofanyika kwa njia ya mtandao wa Bodi ya utendaji, wajumbe hao waliidhinisha pia Mbinu bora za AMECEA za mtiririko wa Misa na Ibada maalum ambazo zitatoa miongozo ya mazoezi ambayo hata hivyo yamekuwa ya kushangaza kufuatia na hatua za kuzuia UVIKO-19 na ambazo ziliwafanya waamini wa kikristo wengi kufuatilia misa mtandaoni.

Mbinu na njia za kuweza kufanikisha tukio

Kwa mujibu wake amemsea “Mazoea haya bora yataongoza hata  mikutano ya washiriki kuzingatia kanuni za Ibada Takatifu kwa wote katika Kanisa Katoliki na mawazo msingi ya utangazaji ili kutoa matokeo mazuri yanayotarajiwa katika mazingira ya maombi na ubora wa maudhui huku waamini wakifuatia liturujia kwa karibu. Akiendelea  Padre Makunde alifafanua hitaji la miongozo ya utiririshaji wa moja kwa moja wa Misa na kuongeza kuwa AMECEA itashirikisha hati kwa wajumbe mabaraza ya maaskofu kwa ajili ya kufuatilia. Zaidi ya hayo, sera na miongozo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) iliyorekebishwa kwa Sekretarieti ya AMECEA pia imeidhinishwa.

Sera ya ICT ya AMECEA imebadilishwa kuenddana na wakati uliowekwa na janga 

Kwa mujibu wa Padre Makunde, amesema sera ya ICT ya Sekretarieti ya AMECEA ya 2015 imerekebishwa kufuatia mabadiliko ya kiteknolojia yanayobadilika kila wakati, habari zinazoibuka, vitisho vya usalama na changamoto na janga la UVIKO-19 ambalo limebadilisha shughuli na sasa wafanyakazi wanaweza kufanya kazi kutokea nyumbani na kazi zaidi rasimi zimefanyika mtandaoni. Mapitio hayo yanalenga kutoa mfumo makini unaoendana na hali halisi ya kiteknolojia na mienendo ya sasa, na ambao utaongoza utoaji wa huduma kwa ajili ya utaratibu kwa njia bora na yenye ufanisi zaidi kuelekea utekelezaji wa majukumu ya Sekretarieti ya AMECEA, alisema Katibu Mkuu  siku ya ya mahojiano. Ijumaa 22 Okotba. Sera hiyo imeanzisha miongozo mipya ikiwa ni pamoja kati ya nyingine, kulinda watoto na uonevu kwa njia ya mtandao, kufanya kazi nyumbani na matumizi ya runinga (CCTV), katika eneo la kazi.

25 October 2021, 14:43