Chama cha Masista wa Kenya (AOSK) wanapongeza juhudi za Wizara ya Afya katika jibu la UVIKO-19 na wanatambua kuwa vita iliyofanikiwa dhidi ya janga hili bado inahitaji msaada wa sekta ya umma na ya kibinafsi. Chama cha Masista wa Kenya (AOSK) wanapongeza juhudi za Wizara ya Afya katika jibu la UVIKO-19 na wanatambua kuwa vita iliyofanikiwa dhidi ya janga hili bado inahitaji msaada wa sekta ya umma na ya kibinafsi. 

Kenya:Watawa nchini kenya wazindua kampeni ya kuzuia UVIKO-19

Chama cha Masista wa Kenya(AOSK)kimezindua kampeni ya kuzuia na uhamasishaji wa uelewa wa UVIKO-19 wa miezi sita ili kuhamasisha jumuiya kupata chanjo na kukumbatia hatua za kinga za UVIKO-19.Vituo 80 vya afya katoliki vinavyoendeshwa na masista nchini humo watashiriki katika kampeni na kutekelezwa agizo la taifa kupitia ufadhili wa Shirika la Hilton.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Kupitia ufadhili kutoka Shirika la Hilton, vituo 80 vya vya afya katoliki vinavyoendeshwa na masista  nchini humo  watashiriki katika kampeni ya kuhakikisha watawa hao wanajimudu kwa kutekelezwa agizo la taifa la huru la UVIKO-19. Katika kipindi cha kampeni ambacho kimeanza tangu Julai hadi Desemba 2021, takriban wafanyakazi wa afya wako mstari wa mbele karibia 1,500 (pamoja na watawa ) ambao watafaidika na mafunzo mbali mbali  ili kujenga uwezo na maarifa yao kwenye UVIKO-19. Kampeni hiyo inatarajiwa kufikia takriban watu milioni 5.

Naye  Sr. Pasilisa Namikoye, Katibu Mtendaji, wa AOSK katika semina ya kuhamasisha wasimamizi wa vituo vya afya 80 kwenye kampeni hiyo amesema  “Kama Chama cha Masista wa Kenya (AOSK) tunapongeza juhudi za Wizara ya Afya katika jibu la UVIKO-19 na tunatambua kuwa vita iliyofanikiwa dhidi ya janga hili linahitaji msaada wa sekta ya umma na ya kibinafsi katika utetezi wa unyonyaji wa chanjo ya UVIKO-19, utoaji wa vifaa muhimu vya matibabu, utoaji wa kinga  na mawasiliano ili kubadilisha mawasiliano”.

Watawa hao katoliki daima wamefanya kazi ya kuboresha na kuongeza upatikanaji wa huduma zmsingi za afya kwa walio katika mazingira magumu zaidi katika jamii. “Tungependa kutumia usambazaji wetu mkubwa nchini kote kuhusika moja kwa moja katika sekta ya afya na ukaribu na umati wa watu kusambaza habari za UVIKO-19 kwa jumuiya zote tunazotumikia na kuhamasisha kuchukua chanjo. Kulingana na Chama hiki cha masisita (AOSK), mpango huu unakamilisha kazi ya majibu ya serikali kuhusu UVIKO-19.

Chama hiki AOSK kitawezesha vituo vya afya 80 ili kutekeleza mipango ya kufikia jumuiya kuhusu uhamasishaji wa chanjo ya UVIKO -19, kutoa mafunzo kwa watoa huduma ya afya juu ya chanjo ya UVIKO-19, kuzuia, kudhibiti na utunzaji wa nyumbani, na kununua vifaa vya PPE, vifaa vya kupima UVIKO-19, mipira za kinga, barakoa za upasuaji, ngao za uso, kujaza mitungi ya oksijeni na oximeter (mashine za SPO).

Kanisa Katoliki nchini Kenya, kupitia majimbo na makanisa ya wanaume na wanawake watawa hutoa huduma za afya kupitia mtandao wa vituo vya afya vinavyojumuisha hospitali 65, vituo vya afya 90, na zahanati 300 na takriban watoa huduma ya afya 5837, ambao 300 wanaendeshwa na masista wakati wengine ni wa jimbo na  parokia. Mitandao ya afya ya AOSK iko chini ya Tume ya Afya Katoliki ya Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya (KCCB), na inashirikiana na Wizara ya Afya kufikia “lengo la Serikali la, kufikia usawa, nafuu, kupatikana na huduma bora za afya kwa wote”.

04 August 2021, 15:19