Iraq inasali kwa ajili ya ujio wa Papa Francisko!
Na Sr. Angela Rwezaula,-Vatican.
Kwa muda fulani tumekuwa tukiishi kwa hofu, lakini pia kwa tumaini, amesema Patriaki wa Babilonia ya Wakaldayo, mara tu aliposikia juu ya ziara ya Papa, Francisko tarehe 7 Desemba iliyopita, na alikuwa ameonesha kuwa ni ishara ya kuzaliwa upya kwa nchi, yaani Noeli mpya. Leo, hii kwa roho hiyo hiyo, Kardinali Louis Raphaël Sako ametunga sala akiomba, kupitia njia za mikondo ya Upatriaki kwamba waamini waisali pamoja wakati wa Misa kila Jumapili kuanzia tarehe 17 Januari 2021. “Bwana Mungu wetu umpe Papa Francisko afya na mafanikio ili aweze kufanikisha ziara hii inayotarajiwa. Bariki juhudi zake za kuimarisha mazungumzo na upatanisho wa kindugu na kujenga uaminifu, kuimarisha maadili ya amani na utu wa kibinadamu, hasa kwetu Wairaq, mashahidi wa matukio ya uchungu ambayo yametugusa”.
Hivi ndivyo inavyoanza sala ambayo, kabla ya kumkabidhi kwa Mama Bikira Maria, ameomba nuru ambayo ni kichocheo kwa wote katika wakati huu kwamba: “Bwana, muumba wetu, angaza nyoyo zetu na nuru yako ili tuweze kuona mema na amani na kuanza kuyatimiza. Kwa njia hiyo maombi ya maombezi Bikira, Mama yetu, ambaye kwa utunzaji wa umama wake amekabidhi Baba Mtakatifu anaandika “Ili Bwana atupe neema ya kuishi katika muungano kamili wa kitaifa, tukishirikiane kidugu kujenga maisha bora ya baadaye Nchi na raia wake”.
Tayari mwanzoni mwa mwezi Desemba mwaka jana, kwa maana ya mwezi mmoja uliopita, Patriaki Sako, akiandika barua kwa watu wa Iraq, alikuwa ameomba kujitayarisha vya kutosha kwa ajili ya kufika kwa Papa ambaye alisema haitakuwa safari ya kitalii au ya anasa badala yake ni hija iliyojaa ujumbe wa faraja kwa wote na kutiwa moyo wakati huu wa kutokuwa na uhakika; na kwamba “lazima tufanye kuwa fursa ya mabadiliko makubwa ili imani na matumaini ndanu yetu iweze kuwa jitihada”.
Francisko anaanza tena kusafiri ambapo atakwenda Iraq tangu tarehe 5 hadi 8 Machi
Hija ya Papa Francis ya kwenda Iraq, kwa mwaliko wa viongozi wa serikali na Kanisa Katoliki huko, ilitangazwa rasmi mapema Desemba iliyopita, ikiashiria kuanza tena kwa safari zilizokatizwa ghafla kwa miezi kumi na tano kwa sababu ya dharura ya kiafya ulimwenguni. Tarehe zilizopangwa ni kuanzia tarehe 5 hadi 8 Machi, na vituo vyake vitakuwa Baghdad, uwanda wa Uru, uliounganishwa na kumbukumbu ya Ibrahim, mji wa Erbil, na Mosul na Qaraqosh katika uwanda wa Ninawi. Siku nne muhimu sana kwa ajili ya ukaribu na watu ambao wameteseka na wanaendelea kuteseka kutokana na vita na ambao pole pole wameona Wakristo wakiondoka nchini humo. Ni safari ambayo Papa Francisko amekuwa akitamani kwa muda mrefu, huku akielezea nia yake tangu 2019 na kila wakati akiongezea maneno yake ya mwaliko wa kujenga nchi hiyo thabiti ya kijamii ambayo inalenga manufaa kwa wote.