Patriaki Pizzaballa wakati wa kuingia katika Kanisa Kuu la Kaburi Takatifu Nchi Takatifu Patriaki Pizzaballa wakati wa kuingia katika Kanisa Kuu la Kaburi Takatifu Nchi Takatifu 

Patriaki Pizzaballa amesisitiza msukumo mpya wa kichungaji unaohitajika

Katika mahubiri yake kwa ajili ya Misa ya Kipapa ya Upatriaki amekumbuka mchakato wa hatua yake katika Nchi Takatifu na changamoto kwa ajili ya Kanisa la Yurusalemu.Ameonesha njia ambayo inahitajika katika uchungaji kwenye Nchi Takatifu ambapo anashauri kuwa na msukumo mpya wa kichungaji.

Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Patriaki wa Killatino huko Yerusalemu Pierbattista Pizzaballa ambaye tarehe 4 Desemba aliingia rasmi kama Patriaki katika Kanisa la Kaburi Takatifu aliadhimsha misa ya Kipapa huku akistoa shukrani kubwa kwa Mungu. Katika mahubiri yake amesema “Katika Eneo hili Takatifu, linataka kunizawadia nguvu, ujasiri na kutoa maisha yangu katika Kanisa hili, kulipenda na kuelekeza na roho ya ubaba na uvumilivu”. Patriaki mpya mawazo yake yamemudisha nyuma ya  mchakato wa safari yake ya utume ambapo, amekumbusha jinsi alivyofika katika Nchi Takatifu miaka 30 iliyopita akiwa kuhani mpya, kuanza mafunzo yake na hatimaye huduma yake ya kichungaji kama Msimamzi wa Nchi Takatifu  ambayo imempa fursa ya kutambua zaidi na zaidi Kanisa la Yerusalemu.

“Sisi tunatembea pamoja na Mungu ambaye tunamjua, lakini ni katika kuelekea wakati  ujao tusioujua amesisitiza Patriaki Pizzaballa  huku akitazama hasa kuhusu kipindi cha sasa, kwani wakati  wetu ujao ni wenye mashaka na ambao  unaweza kusababisha  janga, ambalo lonaendelea, hofu na hisia mbaya. Kwa maana hiyo amesema ni lazima kujikabidhi kwa Mungu anayetambuliwa na ambaye alijifunua wazi kupitia mwanayeYesu ili kupata faraja na nguvu. Lazima  kuwa na matumaini na imani ya  mioyo yetu ikumbuke historia ya pamoja na ya kila mmoja binafsi na kukumbuka mara ngapi tumewza kufanya uzoefu wa uaminifu wa Mungu kwetu sisi, amekazia Patriaki mpya.

Akiendelea na mahubiri yake ameshauri kujikabidhi hata katika Neno la Mungu, kama Petro akiwa katika ziwa la Tiberiade, ambapo kwa hakika hakuficha hisia zake za hofu mbele ya utume wake aliokabidhiwa hivi karibuni na Papa kuongoza Upatriaki wa Kilatino wa Yerusalemu.Kwa maneno yake kuhusu utume huo amesema “ Ninakubali kwa utiii utume huu ambao ninapendelea kuupeleka mbele kwa furaha”. Hakika pia ni Msalaba, lakini Msalaba huzaa matunda ya wokovu kila wakati unapokaribishwa kwa furaha ” Amesisitiza. Akiongelea juu ya Kanisa la Yerusalemu, Patriaki huyo amebainisha kwamba msukumo mpya wa kichungaji unahitajika, na ambao unazingatia maeneo yote na tamaduni tofauti, lakini ambayo inatambua jinsi ya kutafuta na kupata umoja kati ya wote na kwamba kuna shida za kiuchumi na kijamii ambazo zinatakiwa kushughulikiwa, zilizozidishwa na zaidi na janga linaloendelea.

“Tunasubiriwa  kufanya mkutano na Makanisa mengine dada na ndugu Waislam na Wayahudi  ambapo pia tunasibiri kupata hata  neno la wazi na lenye utulivu kutoka siasa ambalo  mara nyingi ni  dhaifu la muda mfupi”, amesema Patriaki Pizzaballa. Kwa maana hiyo Patriaki ameomba waamini kusali kwa ajili ya utume wake na kwa ajili ya Kanisa la Yerusalemu, na akahitimisha mahubiri yake amesema “ tunao uhakika kwamba Mfufuka arambua kwa namna nyingine kutjaza Roho wake na kutufanya kuwa katika Nchi yake Mashuhuda wa kweli wa upendo wake.”

05 December 2020, 15:18