Papa:Askofu Teissier alikuwa mtu wa mazungumzo na amani
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Papa Franciko ametuma salam za rambi rambi, zilizotiwa saini na Kardinali Pietro Palorin Katibu wa Vatican iliyoelekezwa kwa Askofu Paul Desfarges wa Algeria kufuatia na kifo cha Askofu Mkuu Henri Teissier. Katika Ujumbe huo Papa Francisko ameelezea maskitiko yake akifungua siku ambayo ilikuwa inakumbusha Kumbu kumbu ya Mwenyeheri Charles de Foucauld, tarehe Mosi Desemba na hivyo kupata habari za kifo cha Askofu Mkuu mstaafu Henri Teissier, aliyekuwa Askofu Mkuu wa Algeria. Papa Francisko anamwombea kwa Bwana roho yake ya mchungaji mkarimu na ambaye alitambua kwa ujasiri mkubwa na roho ya kiinjili kuishi majaribu ya Kanisa nchini Algeria.
Alikuwa ni mtu wa mazungumzo na amani na alikwenda kukutana kwa heshima na roho ya kidugu watu wa Algeria katika michako ya safari ya maisha yake kwa miaka mingi huku akihudumia katika majimbo ya Orano na Algeri, aliyokuwa amekabidhiwa kichungaji. Katika kuomba kwa Baba kisima cha kila huruma na kumpokea Askofu aliyeagaza dunia katika amani na mwanga wa Ufalme wake na kwa kumkabidhi kwa maombezi ya Mama yetu wa Afrika, Mwenyeheri Charles de Foucauld na watakatifu wafiadini wa Algeria, Baba Mtakatifu anasali kwa ajili ya watu wote walioondokewa na yeye na kwa moyo wote anawatumia Baraka ya Kitume: familia na ndugu wa marehemu, maaskofu wa Algeria, waamini wa Orano wa Algeri na watu wote wanaoshiriki liturujia ya mazishi.
Askofu Mkuu Henri Teissier, alizaliwa Lione kunako mwaka 1929, na alipata daraja la upadre huko Algeri kunako 1955 baada ya masomo yake katika Seminari ya Wakarmeli huko Paris. Alijifunza kiaraba katika Taasisi ya Kidomenicani huko Algeri manmo 1958. Aliteuliwa kuwa askofu wa Orano 1973, baadaye msaidizi wa Algeri wa Kardinali Duval tangu 1981, na 1988 akawa mfuasi wa Kardinali Duval kuwa Askofu Mkuu wa Algeri, mahali alikaa hapo hadi 2008. Baada ya kung’atuka kwa sababu ya umeri wake alishirikisha maisha yake kati ya Ufaransa na Algeri. Ameaga dunia akiwa amezungukwa na ndugu zake katika Hospitali ya Édouard-Herriot, baada ya kupata kiharusi.