Watu wa mali lazima waweze kuishi kwa pamoja kwa amani. Watu wa mali lazima waweze kuishi kwa pamoja kwa amani. 

Mali:Mafunzo kwa walimu toleo la pili 2020 limehitimishwa!

Mpango unaofadhiliwa na Baraza la Maaskofu Italia (CEI) kwa elimu ya waalimu wa elimu Katoliki ambao unatoa mafunzo ya miaka mitatu mitatu kwa toleo sasa la pili kwa mwaka huu 2020 umehitimishwa nchini Mali.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Walimu, wakuu wa shule na washauri wamejadiliana kuhusu elimu ya amani katika shule kwa mantiki ya uhusiano wa mtindo wa kuishi bila kutumia nguvu hasa katika sehemu zenye migogoro. Kozi hii imehitimishwa hivi karibuni huko Bamako nchini Mali. Kitengo cha mafunzo ya toleo la pili  2020 na ambacho kinatazama  Majimbo ya Kayes, Bamako, Sikasso, kimehusisha hata majimbo ya Mtakatifu  San, Mopti na Ségou. Kwa mujibu wa taarifa za Baraza la Maaskofu nchini Mali, huo ni mpango kati ya Kozi zilizoandaliwa kwa ajili ya walimu wa Kitaifa wa Elimu Katoliki ili hatimaye kuhakikisha hupatikanaji wa elimu bora na  shukrani kubwa kwa ufadhili wa Baraza la Maaskofu Italia (CEI).

Kwa kuzingatia kwamba   nchi ya Mali  kila wakati imekumbwa na vurugu, chuki na sintofahamu, Koundia Joseph Guindo, mhusika wa kitaifa wa Mtaala wa Elimu Katoliki amesema kuwa wanaishi wote bila kuwa na usalama. Nchini Mali inahitaji amani. Watu wa mali lazima waweze kuishi kwa pamoja kwa amani. Wakati wa kozi yao, mbinu ya kufundisha kusoma kwa njia ya mtaala na elimu Msingi  pia ilijadiliwa. Washiriki, karibu hamsini, pia walipata fursa ya kushiriki uzoefu wao na kuongeza maarifa yao. Mpango huo unaofadhiliwa na Baraza la Maaskofu Italia (CEI) kwa waalimu wa elimu Katoliki hutoa mafunzo ya miaka mitatu mitatu.

03 October 2020, 16:24