Padre Mauro Gambetti msimamizi wa Conventi Takatifu ametuliwa na Papa kuwa Kardinali. Padre Mauro Gambetti msimamizi wa Conventi Takatifu ametuliwa na Papa kuwa Kardinali. 

Assisi Jimbo linafuraha kubwa kuchaguliwa Padre Mauro!

Katika barua ya Askofu Domenico wa Jimbo la Assisi -Nocera Umbra-Gualdo Tadino ameelezea furaha yake kuhusu kuchaguliwa kwa Padre Mauro Gambetti msimamizi wa Conventi Takatifu Assisi kuwa Kardinali. “Ni vizuri kuona mtoto wa Francis wa Assisi,ambaye kwa sasa ni Msimamzi wa Conventi Takatifu, kwa maana ya moyo wa maisha ya kifransiskani ulimwengunu anaitwa katika shughuli karibu na Baba Mtakatifu".

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican.

Furaha ni kubwa kwa uteuzi Kardinali Mteule  Padre Mauro Gambetti Mfuransisikani Mkoventuali na Msimamizi wa Conventi Takatifu ya Assisi.Wanamshukuru Papa Francisko kwa ishara ya umakini na heshima na mapendo aliyopkea kwa kumteua kuwa Kardinali wa Kanisa takatifu la Roma. Ni katika barua ya Askofu  Domenico wa Jimbo hilo. Katika barua hiyo inasema kuwa “Ni vizuri kuona mtoto wa Francis wa Assisi, ambaye kwa sasa ni Msimamzi wa Conventi Takatifu, kwa maana hiyo katika moyo wa maisha ya kifransiskani ulimwengunu kuitwa ili aweze kujikita  katika shughuli yake karibu na Baba Mtakatifu , kwenye nafasi ya Baraza na msaada ambao ni wa Baraza la  cha makadinali katika kuongoza Kanisa la ulimwengu. Padre Mauro alikuwa na anabaki, kwa muda mrefu iwezekanavyo, kama Kasisi wangu katika Kanisa kuu la Kipapa la Mtakatifu Francis. Pia katika nafasi hii nimekuwa naye kwa ushirikiano wa kiaminifu kwa miaka mingi katika Baraza langu la Maaskofu”.

Askofu Dominico wa Jimbo la Asisisi SSISI -Nocera Umbera-Gualdo Todino akiendelea na ufafanuzi kuhusu uteuzi huu amesema  “Hitimisho la mamlaka yake kama Msimamizi wa Conveti Takatifu  ulitarajiwa katika kipindi hiki, na kila kitu kilionesha uhamasishaji wake katika huduma ya Kanisa. Aina hii ya huduma muhimu sana na ya upendo ambayo Baba Mtakatifu amemwomba kwake yeye ni sababu ya heshima kwake na kwa familia za Wafransiskani, lakini pia furaha kwetu sisi sote, na kwangu mimi kwa njia fulani, kuunganishwa naye na hisia za mapendo na shukrani”, amesisitiza Askofu Domenico.

Chini ya uongozi wa Baba Mtakatifu Francisko, Kanisa leo hii linahisi hitaji kubwa la kufanywa upya kwa jina la “furaha ya Injili” na kusuka  kwa upya roho ya familia, ya muungano na  umoja.  Katika hali ya tasaufi ya kifransiskani ya Padre Mauro  ndiyo tumaini pia la uzoefu wake wa kichungaji katika Kanisa kuu hili  ambalo linawaomba wazawa wa Mtakatifu maskini Francis kuwa katika kila aina ya huduma ya Baba Mtakatifu ambayo atapenda kuwapatia na iwe kwake msaada, faraja na msukumo kwake. Sala yetu kwa ajili yake imehakikishiwa. Lakini akumbuke kuwa Assisi kiukweli inabaki kuwa nyumba yake mara mbili .Mpendwa Kardinali mpya Mauro, tunakupenda.  Na mkumbatio maalum kutoka kwa Askofu wako Domenico.

27 October 2020, 09:26