Gabon:Parokia ya Abeke Ville imetendewa ishara mbaya ya ukufuru!
Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican.
Paroko wa Kanisa la Mamajusi Wafalme huko Akebe Ville, mkoa wa Libreville, nchini Gabon, Padre Benoît Dieme hivi karibuni “ni kama kuchomwa Panga halisi moyoni kuafuatia na tukio lakunajisi Kanisani ambalo limetokea tarehe 12 Septemba 2020. “Kijana asiyejulikana alivunja vipande viwili monstrance ya Sakramenti Takatifu na kuiba chombo kidogo kinachotunza Mwili wa Kristo. Kwa mujibu wa Paroko “Tumepigwa na mshangao mkubwa sana”, alisema na kuongeza kuwashauri waamini waombe pamoja kwa malipizi ya tendo hili zito. “Tumekasirika na kusikitika, lakini tunavumilia”, alisema Padri Dieme. Kwa upande wake, Wizara ya Mambo ya Ndani, kwa maandishi, waliandikia “nalaani tukio hilo kwa uthabiti mkubwa na ninawahakikishia makasisi wa Gabon kuwa tutapata mwanga zaidi juu ya tukio hili la uharibifu”.
Hitimisho la tendo hilo
Kufuatia na tukio hilo hata hivyo kwa bahati nzuri, limepata muafaka kwani haukuwa muda mrefu ambapo Paroko huyo Padre Dieme alipotangaza kuwa mhusika wa tendo hilo la kukufuru amerudi parokiani na kukabidhi Monstrance.
“Kijana ameomba msamaha. Nimembariki pamoja na wazazi wake”. Tumshukuru Mungu kwa sababu Yesu katika Sakramenti ya Ekaristi amerudi katika nyumba yetu” amehitimisha Paroko huyo.