UFILIPPINI#coronavirus.Kanisa la Manila:shughuli za kidini ni huduma msingi!
Sr.Angela Rwezaula – Vatican
Huduma ya kidini ni msingi kwa ajili ya watu wetu, ndiyo wito uliotolewa kwa serikali uliomo katika Barua ya Msimamizi wa Kitume wa Jimbo Kuu katoliki la Manila Ufippini, Askofu Broderick Pabillo. Barua ya Kichungaji iliyopewa jina “Twende mbele” wa hakika Askofu anabainisha juu ya kanuni zinazotumika wakati huu wa janga la virusi vya corona na hasa kwa serikali baada ya kuweka vizingiti vya maadhimisho ya kidini kwa uwepo wa watu kumi tu, bila kuzingatia ukubwa tofauti na uwezo wa maeneo ya kufanyia ibada katika Makanisa hayo.
Wakati huo huo, Askofu katika barua yake amewashauri waamini bado aendelee kuheshimu miongozo iliyoanzishwa na Jimbo Kuu na iliyosasishwa na Idara ya Afya ya nchi hiyo kwani anasema ni muhimu, kwa sababu “kila mmoja wetu lazima azingatie siyo afya ya mtu binafsi lakini pia hata ya wengine”. Kwa njia nyingine msimamizi huyo anahamasiaha kanuni za janga na hasa la kukaa nyumbani kwa wazee au wagonjwa; kuwasaidia wanaohitaji zaidi hasa katika mantiki ya msaada wa Kanisa la umoja kwa ajili ya kushirikiana ili kwa pamoja inawezekana kutembea pamoja katika hali hiyo.
Na kwa upande wa Makuhani, Msimamizi wa kitume jimbo Kuu Manila anabainisha juu ya umuhimu wa kusikiliza mawazo ya waamini wenyewe wakati wa kipindi hiki na ili kuleta pamoja ushiriki hai wa maisha ya Kanisa. Askofu Pabillo amewaachia kila parokia na vyama vya kitume kupanga shughuli zao binafsi katika kipindi hiki kwa kutoa mwaliko wa kuacha nafasi katika “shughuli za uchungaji wa afya hasa kwa wazee na wagonjwa ambao hawawezi kwenda Kanisani. Mungu ni yupo hai hata katika kipindi hiki kipya kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye anazidi kuvuvia na kwa maana hiyo ni vema kung’amua na kumfuata, amehitimisha Askofu Pabillo.