Tafuta

Maaskofu wa Uhispania wameandika ujumbe wao kwa kuongozwa na mada na Maria katika Moyo wa Kanisa wakati wa maadhimisho ya Siku ya maombi iliyofanyika 7 Juni 2020 Maaskofu wa Uhispania wameandika ujumbe wao kwa kuongozwa na mada na Maria katika Moyo wa Kanisa wakati wa maadhimisho ya Siku ya maombi iliyofanyika 7 Juni 2020  

Siku ya maombi nchini Hispania:Na Maria katika moyo wa Kanisa!

Nchini Hispania Jumapili tarehe 7 Juni 2020 Mama Kanisa akiwa anaadhimisha Siku kuu ya Utatu Mtakatifu,Kanisa hilo pia limeadhimisha Siku ya Maombi kwa kuongozwa na kauli mbiu “Na Maria katika moyo wa Kanisa”.

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Na Maria katika Moyo wa Kanisa ndiyo kauli mbiu iliyochaguliwa na Baraza la Maaskofu wa Hispania kuongozwa katika Siku ya Maombi ambayo  imeadhimishwa siku ya Jumapili tarehe 7 Juni 2020 sambamba na Mama Kanisa  kuadhimisha Siku Kuu ya Utatu Mtakatifu. Katika fursa ya siku hiyo, Maaskofu hao wametangaza Ujumbe wao uliotiwa sahini na Askofu Luis Ángel de las Heras Berzal, Rais wa Tume ya Maaskofu kwa ajili ya Maisha ya Watawa ambapo anawaalika watazame Maria kama “mfano wa maisha ya watawa wa ndani kwa  kutafakari   kama Yeye, yaani kukaribisha mwili wao uwe makao ya ibada ya Kristo, katika Kanisa ambalo linawasindikiza watoto wake kwa upendo wa umama kila wakati, hasa nyakati zile ngumu.

Kutafakari ni maisha yaliyofichwa na yenye kuzaa matunda katika ulimwengu

Kama Bikira Maria, katika Jumuiya kiukweli maisha ya ndani yabaki mafichoni kwa yote na kila kitu lakini katika uwepo hai  kwa yote na kila kitu.  Hakika, Mama wa Yesu ni “kumbukumbu ya kwanza ya upendo wa Mungu katika  Mwana na maisha ya kutafakari ni wito wa  upendo wa Yesu katika Kanisa”. Uwepo wa kutafakari, kwa mujibu wa Maaskofu wa Hispania ni maisha yaliyofichwa na yenye kuzaa matunda katika ulimwengu, ambao unaonyesha mwanga wa Mungu, hasa wakati giza linapoukumba ubinadamu”.

Kuna aina tatu ya maisha ya kutafakari kwa mujibu wa maaskofu

Maaskofu katika ujumbe wao hata hivyo wanabainisha kuwa kuna sifa tatu za kutafakari na iliyo ya kwanza ni kulinda kwa dhati ukweli wa kiini cha imani ambayo ni upendo wa Kristo. Kwa hakika, tafakari inadumisha uhai wa imani kwa Mungu  ambaye, kwa upendo wetu, katika ukimya na ubaridi wa usiku, katika kona ya kimaskini kabisa ya ulimwengu huu, amejifanya mtoto kwa ajili ya wokovu wa wote.

Tafakari inatia moyo wa kuwa na matumaini bila kuchoka

Sifa ya  pili  ya kutafakari ni kwamba uwepo wa tafakari unatia moyo bila kuchoka kuhusu tumaini kuu la Kanisa, ambalo ni huruma ya Baba, kwa sababu ni shukrani kwa watu waliowekwa wakfu na kwamba unaamsha ule uvumilivu na kuhifadhi ambaye anajua kuwa amekaribishwa kwa moyo wenye huruma ya Mungu Baba katika kila hali, hata katikati ya mateso makubwa kama haya ya sasa  yaliyosababishwa na janga la virusi vya corona.

Maisha ya wakfu uangaza  ulimwengu furaha ya kuishi Injili

Hatimaye sifa ya tatu ya maisha ya kutafakari yaliyowekwa wakfu, kama  Bikira Maria, yanaangazia ulimwengu ile  furaha ya kuishi kwa mujibu wa Injili na neema ya Roho na kama Bikira  Maria katika  harusi  Kana, alitoa divai ya Habari Njema  katika ulimwengu, katika kubadilisha kila siku matarajio mazuri ya karamu ya Ufalme wa Mungu ”.

08 June 2020, 12:41