Martinez:Mwongozo wa Katekesi ni ufupisho wa huduma ya Papa!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Bwana Salvatore Martinez, rais wa Chama cha Wakarismatiki Katoliki na mshauri wa Baraza la Uhamasishaji wa Uinjilisha Mpya, katika mahojiano na Vatican News ametumia kilelezo kuwa Hati ni ‘magna charta’kwa ajili ya changamoto za Milenia ya Tatu katika ufafanuzi wake kuhusu Mwongozo mpya wa katekesi uliochapishwa na kutangazwa hivi karibuni tarehe 25 Juni 2020. Bwana Martinez amesema, Mwongozo mpya wa Katekesi ni kielelezo waziwazi cha mafundisho ya Papa Francisko. Hati hiyo ambayo pia inasisitiza hata dharura ya kujitoa kwa kila mtu aliyebatizwa ili kueneza Injili kwa kutumia kanuni tatu msingi:huruma, mazungumzo na ushuhuda kwa mujibu wa Martinez amethibitisha huo “ ni utaratibu wa mawazo ya Papa na utayari wake katika kutoa huduma huku akishuhudia. Na hii ni kwa sababu changamoto kubwa za uinjilishaji mpya wa Milenia ya Tatu zinaoneshwa kwa wakati huu unaofaa na kuwa nguvu na ukweli. Mwongozo huo wa katekesi pia ni aina ya kitaalimungu, na kikanisa hasa katika msamiati wa Papa Francisko. Vile vile unadhihirisha njia inayofaa kwa mahitaji ya wakati wetu, katika changamoto zilizo na dalili nyingi, kiasili, na kutoa mwelekezo, wa kufanya utume kimwendokasi na kwa imani.
Katika ufafanuzi wa Bwana Martinez anasema Hati hiyo inaonesha wazi mada kuu ya kuwa na imani thabiti. Imani ni maisha na inatakiwa hasa katika karne hii, mwanzoni mwa milenia mpya na kuongeza kusema, baadaye kuna uenezaji wa imani, yaani mazungumzo na tamaduni mbalimbali, mielekeo ya sasa ya mawazo. Tatu, kuna mada ya utamaduni wa mazungumzo, ya kukutana, ambayo ni nyeti kwa upande wa Papa Francisko. Yote hayo hii yamewekwa vizuri na lugha inayoeleweka na kujikitana ndani ya muhtasari wa huduma ya kipapa kuanzia na Wosia wake wa Kitume ‘Evangelii Gaudium’, yaani Injili ya Furaha.
Hati ambayo inakumbusha kuwa kila mbatizwa ni mwajibikaji wa kueneza Injili kwa njia rahisi za mawasiliano, Bwana Martinez anasema kuna muktadha wa jumla ambao labda hadi jana tumeelezea hali halisi, kama vile ulimwengu wa digitali au utandawazi. Huduma ya kichungaji kwa sasa inataka kutoa umakini kwa wale ambao wako katika mantiki hii muhimu na ambayo kila kitu hufanyika na kutumiwa katika maisha yao, kwa maana ya kwamba ni mahali ambapo wanaume na wanawake wanahitaji Injili ya Kristo. Mwongozo wa katekesi aidha unatukumbusha kwamba uinjilishaji haujafanyiki kwa ajili ya kupokea sakramenti tu. Ni katekesi ya kweli na siyo kuwa inapendekeza kukutana na Yesu peke yake lakini pia inayotuwezesha kuzaa matunda, kuongea na kumpeleka Kristo kwa watu wote. Ni uhusiano mkubwa uliopo kati ya malezi na uinjilishaji. Amesisitiza Bwana Martinez.
Mwongozo wa Katekesi pia unaweka wazi kutazam familia kuwa chombo msingi kuanzia hasa katika mazungumzo ya katekesi ya kwanza. Unakumbusha wazi kuwa familia ni fursa ya uinjilishaji ulio hai. Familia siyo mada ya katekesi tu, lakini ni mahali ambapo imani inarithishwa na kuishi na kujiandaa kuishuhudia. Injili inazaliwa katika familia. Mwongozo wa Katekesi unapendekeza hata mada ya uhusiano wa kizazi na kizazi cha kibinadamu na kwamba katekesi iwe kichocheo kinachounda ili kwamba kuna shughuli mpya ambayo inaanzia kutoka kwa watoto hadi kufikia hadi wazee, na sehemu muingine kama vile kwa wafungwa, wagonjwa , kazini , kila eneo lolote ni sehemu muafaka wa kueneza na kutangaza Injili ya Bwana.
Katika mwongozo wa Katekesi kuna sehemu ambayo inatazama maparokia, harakati na vyama vya kitume, mashule katoliki. Harakati na vyama vya kitume vinahitaji kupokea msukumo mpya. Katika changamoto ya uinjilishaji mpya hakuna shaka kuwa wana jukumu la kusisimua. Ni muhimu kwamba Mwongozo huu chini ya mtazamo wa kitaalimungu -kichungaji, unathibitisha tena mahali pa harakati za kanisa katika makanisa maalum na baadaye kushiriki mazungumzo na ulimwengu. Harakati hizo zinafanywa na watu walei na katika umwengu unawasubiri wao kushuhudia Injili hata kwa njia ya mafunzo ya kielimu ya kupyaisha yanayohusishwa na karama nyingi zilizowekwa na Roho Mtakatifu.