2020.06.02 picha ya George Floyd iliyochorwa ukutani 2020.06.02 picha ya George Floyd iliyochorwa ukutani 

MAREKANI.Pax Christi:Tujikite katika haki kwa ajili ya George Floyd,siyo kuhukumu kwa waandamanaji!

Wito kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Pax Christ,Marekani mara baada ya kifo cha George Floyd Mmarekani mweusi kwa kukabwa koo na afisa polisi na kwamba lazima kutafuta haki kwa ajili yake na siyo kuhukumu waandamanaji.Hii inatakiwa kufanya kila liwezekanalo kuzuia uhalifu huu usirudiwe.Umakini unapaswa upewe kipaumbele cha haki kwa wale wote ambao wameuwawa.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Bwana Bob Shine, Mwenyekiti wa Baraza ka Kitaifa la “Pax Christ” yaani  Amani ya Kristo” nchini  Marekani ameandika katika tovuti ya Chama hicho kufuatana na maandamano makali yanayoendelea ya kupinga yaliyoibuka katika miji yote ya Nchi, mara baada ya kuuawa kwa George Floyd  katika uhalifu wa afisa wa polisi huko Minneapolis. “Mtu hapaswi kuhukumu kinachotokea katika maandamano mengine, lakini basi ni kujiuliza ni nini kimekuwa kikijitokeza kwa watu weusi katika nchi hii mara kwa mar ana zaidi kupambana na watu weusi”.

Kwa mujibu wa Shine amesema, “kile ambacho tunatakiwa kukumbuka na kile ambacho hatuwezi kamwe kupoteza hapo ni kwamba mtu mweusi George Floyd, aliuawa na afisa wa polisi baada ya kukamatwa kwa tuhuma za uhalifu wa kulipa kwa kutumia noti ya bandia ya dola 20.  Mtu huyo alifariki baada ya afisa wa polisi kuibana shingo yake  kwa  goti kwa karibu  dakika tisa hata wakati ambapo Floyd alikuwa akiomba angalau aweze kupumua. Na wakati huo huo Polisi wengine walibaki wakatizama tu. Tukio kama hili limejirudia lenyewe na kwa njia tofauti,  zaidi ya mamia ya miaka katika nchi yetu. Watu weusi wanakabiliwa na vitisho vikali kila siku, na ukweli ambao unaoonekana wazi katika matendo ya polisi wakati wa maandamano.”

Kiongozi huyo Shine amesisitiza kwa kutazama waandamanaji weusi katika wakati wa Trump na virusi vya corona, kwenye makala ya ‘Los Angeles Times’, Kareem Abdul-Jabbar, mmoja wa wachezaji wakubwa wa NBA na mmoja wa wanaosikiliza sauti za Kiafrika zaidi nchini  ameandika kuwa “tunapaswa kuona kuwa watu wamesukumwa sana hadi ukomo, siyo kwa sababu wanataka bar na  saluni  za uzuri zilizo wazi, lakini ni kwa sababu wanataka kuishi. Kupumua”. Kwa maana hiyo, kiongozi huyo wa Pax Christ Marekani kwa kuhitimisha anasisitiza kwamba  “Lengo letu na hapa ninazungumzia kwa namna ya pekee kwa wazungu kama mimi, ni kufanya kila liwezekanalo kuzuia uhalifu huu usirudiwe. Umakini unapaswa upewe kipaumbele cha haki kwa wale wote ambao wameuwawa.

03 June 2020, 15:22