SENEGAL#coronavirus:uamuzi wa Mfuko wa Caritas kwa waathirika wa kiuchumi!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Mfuko Katoliki wa dharura wa Caritas uliokuwa umezinduliwa mwezi Machi iliyopita kwa ajili ya kusaidia watu wa Senegal waliokuwa wamepata pigo la dharura iliyosababishwa na mvua, kipindi cha baridi au mafuriko na kuongeza uwezo wa kukabiliana na hali halisi iliyokuwapo wakati ule, kwa sasa, wameamua mfuko huo kuuelekeza katika mgogoro wa afya kijamii wa sasa.
Kutokana na dharura ya sasa ya kiafya katika janga la virusi vya corona, Mfuko Katoliki wa dharura kwa upande wa Caritas nchini Senegal utawasaidia watu wenye shida sana na zaidi wazee ambao wanajikuta katika hali ya matatizo makubwa kutokana na janga la Covid-19. Kwa mujibu wa taarifa iliyotangazwa na vyombo vya habari mahalia, pia wamesitisha ukusanyaji wa fedha ambao ulikuwa uwaunganishe majimbo yote ya Nchi kwa ajili ya kusaidia watu wenye shida zaidi.
Lengo la Caritas ni lile la kuwasaidia hasa wale ambao hawana zana na mahitaji msingi kwa sababu ya mgogoro wa kiuchumi- kijamii uliosababishwa na dharura ya kiafya. Mfuko wa fedha ulikuwa umekusanya hadi sasa zaidi ya milioni 10 za kifranki na sasa ambazo zitatumika kwa ajili ya matumizi ya familia zilizo na shida sana. Aidha katika taarifa hiyo inabanisha kuwa miundo ya majengo ya kiafya ya Kanisa Katoliki mahali ambamo wamelazwa wagonjwa wa virusi vya corona watapokea misaada mingine na wakati huo huo kandoni mwa misaada kwa ajili ya kusaidia dhaura ya vyakula kwa ajili ya miezi ijayo.
Hatimaye wanashukuru sana kwa wale ambao hadi sasa wameweza kuonesha mshikamano wao na hivyo Caritas nchini Senegal, inawaalika watu wote kuendelea kujikita kwa dhati ili kuwasaidia maskini zaidi katika kipindi hiki kigumu na kuendelea kusaidia Mfuko Katoliki wa dharura ili upate kuendelea kwa kina kisaidia walio athirika zaidi.