Katika kipindi hiki ambacho Makanisa yamefungwa,Askofu Mkuu Kaigama wa Jimbo Kuu Katoliki  Abuja,Nigeria anaawalika waamini kuendelea na sala ya kina na matendo ya huruma kama wakristo wa kwanza Katika kipindi hiki ambacho Makanisa yamefungwa,Askofu Mkuu Kaigama wa Jimbo Kuu Katoliki Abuja,Nigeria anaawalika waamini kuendelea na sala ya kina na matendo ya huruma kama wakristo wa kwanza  

Nigeria#Coronavirus:Makanisa yamefungwa kipindi hiki lakini siyo mioyoni mwetu!

Askofu Mkuu Kaigama wa jimbo kuu Katoliki la Abuja nchini Nigeria wakati wa Misa Jumapili ya Huruma amesema kuwa licha ya makanisa kufungwa,lakini virusi vya corona havijazuia kuwa na matendo yote ya kiroho kama vile sala za kina,kusoma Neno la Mungu na kutoa upendo kwa jirani.Ametoa ombi kwa waamini wote nchini humo kuwasaidia wenzao walio katika hali ngumu.

Na Sr. Angela Rezaula – Vatican

Katika Misa ya Dominika ya Huruma ya Mungu  Jumapili 19 Aprili 2020 kwa upande wa Kanisa Kuu la Abuja nchini Nigeria iliyotangazwa moja kwa moja kwa waamini kupitia ukurasa wao wa  Facebook, Askofu Mkuu Ignatius Kaigama, wa Jimbo Kuu hilo alisema kuwa “Virusi vya corona vimesababaisha kufungwa makanisa  yetu lakini mioyo yetu lazima ibaki imefunguliwa kwa imani na  matumaini katika Ufufuko, Huruma ya Mungu na katika upendo wa mmoja na mwingine”.

Askofu Mkuu wa Abuja aliwaalika waamini kubaki wameungana kiroho hata kama wametengana kimwili. “Kanisa siyo mihimili ya majengo tu"  lakini pia watambue kuwa wao ni  “hekalu la roho Mtakatifu”. Askofu Mkuu kwa kutazama kupindi hiki cha vizuizi katika dharura hii ya kiafya amethibitisha kuwa havikuweza kuwazuia kuadhimisha kwa furaha hata Pasaka  hii maalum. Licha ya usambaaji wa virusi vya corona na kupigisha magoti ulimwengu mzima, “havikuwa na uwezo wa kugandisha au kuzika imani yetu  na licha ya umbali uliopo wa kijamii haukuweza kuondoa msimamo wa Kanisa na kuondoa ule upendo kwa wengine kama ilivyokuwa ikijitokeza kwa wakristo wa kwanza”.

Askofu Mkuu Kaigama vile vile amebainisha ni kwa jinsi gani kipindi  hiki licha ya kuwa na ugumu lakini imekuwa kama fursa ya kibinadamu. Hii ina maana kwamba  kipindi hiki cha  pekee kimetoa  fursa kwa wakristo kuanza kwa upya namna ya kupenda na kusaidiana mmoja na mwingine; kukuza na kutunza ule ukimya wakati wa tafakari na kuwa na maisha ya kina zaidi ndani ya mioyo  huku wakijisomea zaidi Neno la Mungu na kusali kwa kina. Kwa  maneno mengine Askofu Mkuu anabainisha ni kama “kuonyesha ile sababu ya imani yetu kwa ngazi iliyo ya juu zaidi”.

Kwa kufafanua anabainisha kuwa ni kwamba suala la kuabudu sio la kijuu juu, lakini ni matendo hai, ya  dhati ambayo “Yesu alitufundisha juu ya upendo, amani, huduma na msamaha”. Kwa maana hiyo  ndipo alitoa wito wa  kuwa na mshikamano hasa kwa wale wanao hitaji zaidi katika nyakati hizi ngumu. Hasa akiwaomba wanajimbo kuu kusaidia wanageria wengi ambao katika kipindi hiki wamebaki bila msaada kutokana na janga la corona.

23 April 2020, 14:57