Vinajana wakatoliki nchini Indonesia wanaalikwa kuwa makini kusaidia maskini na katika mazingira magumu wakati huu wa  kuenea  kwa coronoavirus-19 Vinajana wakatoliki nchini Indonesia wanaalikwa kuwa makini kusaidia maskini na katika mazingira magumu wakati huu wa kuenea kwa coronoavirus-19 

INDONESIA #coronavirus:Askofu wa Ketapang ashauri vijana wawe mstari wa mbele kusaidia masikini zaidi!

Katika kukabiliana na janga hili la coronavirus-19,Askofu nchini Indonesia anawashauri vijana wawe mstari wa mbele katika ubunifu na kuwasadia maskini na watu wenye kuhitaji.Anawaamini kwa kutumia nyzo zote za kisasa na mitanadao ya kijamii wanaweza kufanya kitu kama ambavyo wamekwisha fanya katika harakati za kulinda mazingira.

Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican

Katika Barua kwa ajili ya Tume ya vijana ya Baraza la maaskofu nchini Indonesia   iliyoangazwa tarehe 31 Machi 2020 inasema: “kuweni makini na kusaidia watu masikini na walio katika mazingira magumu, ninyi wenyewe  na familia zenu, kwa kutumia zana na fursa za njia za mawasiliano kwa ajili ya kuwasadia wengine ili wakidhi mahitaji yao. Katika barua hiyo kwa mujibu wa Shirika la habari UCA News, askofu anawaalika  vijana wakatoliki wawasaidie masikini zaidi na wawe wabunifu katika mapambano dhidi ya Covid-19..

Vijana fuateni hatua zote zilizochukuliwa 

Askofu wa  Ketapang, katika Wilaya ya  Kalimantan  magharibu anawakumbusha vijana kufuata hatua zilizowekwa ili kuzuia maambukizi yaani wakae  nyumbani kuzuia usambaaji zaidi na kufanya mikutano yao kupitia mitandao na kuwa makini katika jamii, ili kuweza kuruhusu wahudumu wafanye shughuli yao katika huduma kwa wale tu  wenye kuhitaji matibabu muhimu ya dharura. Na zaidi anawashauri wasiache kamwe hata mmoja peke yake na wasiache hata mmoja ahisi kudharauliwa katika kipindi hiki kigumu.

Ni wakati sasa wa kufanya kila liwezekanalo 

Ni kipindi chenu sasa  cha kufanya lolote liwezekanalo ulimwenguni na vizuizi vya kimwili haviwezi kuwa vizingiti . Kwa njia ya ubunifu vijana wanaweza  kuwa viongozi wa mstari wa mbele katika hali hii na wanaweza kushinda kwa pamoja kipindi hiki kigumu, anaandika asikofu. “Ni wakati sasa kwenu kugeuka kuwa mstari wa mbele kwa kuwa mifano halisi ambayo wagonjwa, walemavu na maskini wanaweza kupata chakula cha bure”.

Vijana ni wabunifu, wanaweza kama ambavyo tayari katika mazingira

Aidha Askofu anaamini kwamba kile ambacho vijana wanaweza kutafakari ni kama kile ambacho wao tayari wanafanyana kwa ajili ya mazingira, kwa ajili ya Kanisa, jumuiya ya kimataifa, na wanaweza kusaidia maskini waliokumbwa na virusi na wanaweza kufanya kwa namna ya ubunifu na kutumia uwezekano wa njia zote za kisasa. Nchini Indonesia takwimu ya maambukizi  ya covid-19 tarehe 31 Machi 2020 ilikuwa ni 1,528 na vifo 136.

02 April 2020, 09:37