Siku moja kabla ya sherehe za uhuru wa Ghana, umefanyika uzinduzi wa ujenzi wa Kanisa Kuu la Kidini katika mji Mkuu wa Ghana, ishara ya umoja wa Taifa hilo. Siku moja kabla ya sherehe za uhuru wa Ghana, umefanyika uzinduzi wa ujenzi wa Kanisa Kuu la Kidini katika mji Mkuu wa Ghana, ishara ya umoja wa Taifa hilo. 

Ghana:Uzinduzi wa Ujenzi wa Kanisa Kuu la Kidini ni ishara ya Umoja wa Taifa!

Hivi karibuni imefanyika hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa Kanisa Kuu la Kidini katika Mji Mkuu wa Ghana kwa kuweka jiwe la msingi lilitolewa nchi Takatifu Yerusalem.Nia ni katika kuunda ishara ya umoja wa Nchi.Hafla hiyo ilifanya siku moja kabla ya kuadhimisha miaka 63 tangu nchi hiyo ijipatie huru wake.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Mji mkuu wa Ghana hivi karibuni utaona ujenzi wa Kanisa jipya  Kuu la kwanza Kitaifa kwa ajili ya kidini  ambalo ni ishara ya umoja wa Nchi hiyo na ambao ni mpango wa ushirikiano kati ya  Serikali na viongozi wa Kidini katika Nchi hiyo, miongoni mwa viongozi wa Kidini ni Askofu Mkuu mstaafu Charles Palmer – Buckler  wa Jimbo Kuu Katoliki Accra. Shughuli za ujenzi huo limezinduliwa rasmi tarehe 6 Machi katika maadhimisho ya mwaka wa 63 wa Uhuru wa Ghana. Siku moja kabla ya siku kuu  ya Huru kwa mujibu wa Shirika la Habari Katoliki, walifanya hafla fupi ya  kuweka jiwe la kwanza la msingi kutoka Nchi Takatifu Yerusalem. alilokabidhi Balozi wa Israeli Bwana Shab Coope kwa Rais  wa nchi ya Ghana, Bwana Nana Addo Dankwa Akufo- Addo ambaye ni mdau mkubwa wa kuanzisha tukio  la ujenzi huo na ambaye mwanzo alikuwa amesema kwamba “ni shukrani kwa Bwana kwa ajili ya baraka na neema ambayo taifa hili limepokea”. Katika  hafla hiyo kulikuwa na viongozi wawakilishi msingi wa mamlaka ya raia na kidini.

Kanisa Kuu hili la Muungano wa Kidini  Kitaifa litakuwa na mchanganyiko wa ujenzi wa kisasa ambao utawakilisha ishara za kikristo na nyingine za urithi wa utamaduni mahalia na ambalo litaweza kuwa na uwezo wa nafasi ya watu elfu tano kwa mujibu wa mkandarasi wa ujenzi, Bwana David Adjaye Obe. Jengo hili pia litakuwa na vikanisa vidogo vidogo vya  ndani; kisima cha ubatizo na jumba la maonyesho ya Biblia; shule ya muziki na sehemu  ya nafasi za picha za kisanii. Yote hayo yametafakariwa kwa kina kama ishara za umoja, maelewanao na roho ya watu wa Ghana. Kanisa Kuu hilo litakuwa ni eneo la kitaifa  nchini Ghana ambapo waamini wake  wote wa madhehebu yote ya kikristo katika nchi wataweza kuungana kwa pamoja katika kuabudu, kusifu, kutafakari na kuadhimisha liturujia  na ibada za mazishi . Aidha Kanisa kuu hili litakuwa linatumika kufanya  maadhimisho rasmi ya misa za mazishi kitaifa na sherehe mbalimbali za kutoa shukrani. 

10 March 2020, 14:22