Coronavirus:Albania yaikumbatia Italia kukabili dharura!
Na Sr. Angela Rwezaula-Vatican
Mlipuko wa virusi vya corona (covid-19) kwa sasa imezunguka dunia nzima na kufanya kila nchi kuanza kukumbizana katika harakati za kuzuia, kutibu na kushinda matatizo ya kiafya ambayo yanaikumba nchi zote zenye waathrika waliolazwa hospitalini. Katika hilo, hisia shukrani zimewaendea kwa ishara nyingine tena ya nchi ya Albania ambayo imeamua kutoa msaada wao kwa Italia ili kukabiliana kuzuia na kutibu wagonjwa wa covid-19.
Hawa ni madaktari na manesi therathini ambao tayari wameshafika nchini Italia katika kusaidia shughuli zote mahospitali mbalimbali ya dharura inayoendelea. Ni ishara ambayo imependezwa na wengi sana na kuwa na utambuzi kwa upande wa watu wa Italia. Tangazo hilo limetolewa na Waziri Mkuu wa Albania, Bwana Edi Ramana.
Kwa mujibu wa maoni yake ni kuonyesha shukrani ya ule uhusiano mwema wa kidugu na urafiki kati ya nchini hizi mbili na kukumbusha jinsi gani Tirana mji mkuu wa Albania hauwezi kamwe kusahau msaada uliotolewa kutoka Roma wakati wa kipindi cha vita ya wenyewe kwa wenyewe kunako mwaka 1990, ambapo wazalendo wengi wa Albania walikimbia vurugu na ghasia wakapokelewa nchini Italia.
Vatican News, akihojiana na Askofu Ottavio Vitale askofu wa Albania karibu miaka 30 hivi amesema ishara ya Waziri Mkuu wa Albania Bwana Rama ni jambo ambalo ni zaidi ya ishara ya ushirikishano kati ya nchi zilizo karibu. Hii ina maana ya ishara ambayo inawakilisha taadhari kwa Ulaya, ambayo kwa muda huu imekumbwa na matatizo kwa ujumla na ambayo bado hawajaweza kupata suluhisho la pamoja ili kukabiliana na dharura ya covid-19. Ishara kama hizi kwa ujumla Askofu amehitimisha zinapaswa pia zitawale ndani ya mioyo ya wazalnedo wa nchi zote mahalia.