Australia:Querida Amazonia inawatia moyo na changamoto kwa Kanisa la Australia!
Na Sr Angela Rwezaula – Vatican
Askofu Mark Coleridge Rais wa Baraza la Maaskofu Australia, akielezea juu ya Wosia wa Kitume wa Papa Francisko baada ya Sinodi “Querida Amazonia”, iliotangazwa tarehe 12 Februari 2020 anasema kuwa hati hiyo haitazami Kanda moja tu ya mbali duniani, lakini ina mambo mengi ya kusema hata kwa Kanisa la Australia. Askofu amesema: “Amazonia iko mbali sana nasi lakini matatizo yake yanafanana nasi”. Kwa namna ya pekee, “masuala muhimu yaliokabiliwa katika Sinodi na Hati ya Kipapa, kuhusu utamaduni wa watu asilia na uwelewa fungamani wa kiekolojia, vinastahili umakini na kipaumbele katika muktadha wa Australia”, amesisitiza Askofu.
Kama ilivyo Amazonia, hata Australia wanafanya uzoefu wa kwa namna ya janga kubwa la motot, uharibifu wa mazingira ya asili na si tu katika mazingira lakini pia hata kwa wanyama na bayoanuai, juu ya jumuiya na kwa watu wengi. ‘Querida Amazonia’, anathibitisha Askofu wa Brisbane kama alivyosisitiza Papa Francisko kwenye wosia wake wa Laudato Si, kuhusu uwajibikaji wa Kanisa wa kutunza nyumba yetu ya pamoja , ambao unahitaji ujasiri katika mafundisho ya kipapa katika mantiki maalum”.
Kwa mujibu wa Askofu Coleridge anaonesha umakini wa Papa kuhusu utamaduni wa watu asilia katika Amazonia ambao pia unatazama kwa namna ya pekee hata Australia kwa kufikiria hali mbaya ya ukosefu wa maendeleo ili kuweza kukidhi pengo kubwa lililopo la uchumi kijamii , kati ya watu wa asili na wasio asili nchini Austalia. Kutokana na kesi kama hiyo ndiyo changamoto kubwa na kuwatia moya Kanisa la nchi yao pia. Rais wa Baraza la Maaskofu Austalia pia amebainisha juu ya mwaliko wa Papa Francisko kwa maaskofu wote duniani kuweza kusaidia Kanisa la Amazonia ili kuondoa pengo kubwa lililopo la ukosefu wa makuhani.
Kama Australia anasema wazo hili linaweza kuanza kupitishwa siku, wiki , miezi au miaka bila hata waamini kupata Ekaristi takatifu na ni ngumu kutambua. Watu wa Amazonia wana uchungu mkubwa. Vile vile Askofu Mkuu ameelezea juu ya umuhimu wa huduma ya walei ambao wako mstari wa mbele katika masuala ya Kanisa, na nafasi ya watawa na mashemasi wa kudumu katika Kanisa la Amazonia. Ikiwa kila mmoja anajikita kuwa sehemu na kufanya sehemu yake, ushuhuda kwa namna hiyo wa Kanisa unakuwa na nguvu zaidi.