Nembo ya Jumuiya ya Kiekumene kwa ajili ya mkutano wao wa kimataifa unaotarajiwa kufanyika jini Torino nchini Italia kuanzia tarehe 28 Desemba 2020 hadi Mosi, Januari 2021 Nembo ya Jumuiya ya Kiekumene kwa ajili ya mkutano wao wa kimataifa unaotarajiwa kufanyika jini Torino nchini Italia kuanzia tarehe 28 Desemba 2020 hadi Mosi, Januari 2021 

Onyesho la Sanda ya maziko ya Yesu kwa mara nyingine huko Torino Italia!

Askofu Mkuu Cesare Nosiglia wa jimbo kuu Katoliki la Torino nchini Italia amewakilisha kwa vyombo vya habari juu ya Toleo la 43 la shughuli za Jumuia ya Kiekumene ya Taize inayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 28 Desemba 2020 hadi Mosi Januari 2021.Katika maandalizi hayo familia zitakaribisha karibia vijana 15elfu na kutawekwa wazi Onesho la Sanda ya Yesu.

Na Padre Angelo Shikombe;- Vatican

Askofu Mkuu Cesare Nosiglia wa Jimbo la Torino ametoa tangazo la kufanyika tena maonyesho ya kipekee juu ya Sanda ya maziko ya Yesu Kristo  yanatarajiwa kurudiwa tena mnamo tarehe 28 desemba 2020 katika Kanisa Kuu la Torino nchini Italia. Hija hiyo inaongozwa na  kaulimbiu: “Hija ya imani duniani” na mbayo imepata mwitikio chanya kutoka jumuiya mbalimbali hapa nchini Italia.  Ameyasema hayo katika mkutano wa maandalizi ya maonyesho hayo yanayowalenga vijana mahujaji. Aidha Askofu mkuu Cesare Nosiglia amesema Jumuiya ya Kiekumene ya kimataifa Taizé imeichagua sehemu ya Torino nchini Italia kuwa sehemu muafaka ya hija yao  itakayoanza tarehe 28 Desemba 2020 na kumalizika Januari mosi, 2021. 

Naye mwandishi wa Vatican News  Robin Gomes ametaarifu kuwa, Maonyesho haya ya tano tangu yaanze kufanyika mnamo mwaka 2000 yanatarajiwa kuwa na ufanisi mkubwa japokuwa Torino hakuwahi kuwa na historia ya mafundisho kikanisa. Kwa mara ya mwisho maonyesho hayo yalifanyika kunako tarehe 24 Juni 2015 katika Kanisa kuu la Torino nchini Italia.

Baba Mtakatifu Francisko mnamo tarehe 21 na 22 Juni 2019 alisali kwa muda mfupi katika Grotto hiyo na akiwa katika Misa na kufafanua juu ya Groto hiyo kuwa ni  alama ya upendo wa Kristo. Grotto  inayohifadhi Sanda hiyo  Katika kanisa kuu imekuwa kivutio kwa watu wengi na hasa kwa wenye mahangaiko. Mtakatifu Yohane Paulo II alitembelea sehemu ya Grotto hiyo mnamo 1998 na kuona mazingira maajabu ya kimazingira ambayo yanavuta kufanya utafiti ili kuona kama kweli masalia ya nguo za maziko ya Yesu Kristo zilikuwa mahali hapo. 

Baba Mtakatifu Mstaafu Benedicto XVI alielezea kuwa alama hiyo imeandkwa kwa damu ya mtu aliyesulibiwa.  Askofu Mkuu Nosiglia alibaini eneo hilo kuwa linafaa kwa hja ya vijana wa Italia wanaotokea maeneo ya Piedmonte. Askofu Mkuu Nosiglia amefanya mkutano mnamo tarehe 3 Januari 2020 huko Torino, Italia ili kuandaa hija hiyo. 

05 January 2020, 11:13