Tafuta

Maaskofu wa Kanda ya Afrika katika maziwa makuu wanaombea amani katika katika nchi zao mara baada ya mkutano wao mkuu wa hivi karibun.i Maaskofu wa Kanda ya Afrika katika maziwa makuu wanaombea amani katika katika nchi zao mara baada ya mkutano wao mkuu wa hivi karibun.i 

Maaskofu Kanda ya Afrika:Ombi la amani katika kanda ya Maziwa Makuu!

Kamati ya kudumu ya,Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Afrika ya Kati (Aceac) wamekabiliana na hali halisi inayowasumbua katika kanda ya Afrika kwa ajili ya kupata amani ya kudumu katika Kanda ya maziwa makuu na tafakari ya Motu Proprio ya Papa Francisko “Vos estis lux Mundi” kuhusu ulinzi wa watoto na watu waathirika katika Kanisa.Mkutano wao umefanyika huko Bukavu,Congo drc.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Hali halisi ngumu ya uchungaji kijamii katika Jamhuri ya Kidemokarasaia ya  Congo, ya Rwanda na Burundi, jitihada za amani ya kudumua katika Kanda yote ya Maziwa Makuu na Motu Proprio ya Papa Francisko “Vos estis lux Mundi” kuhusu ulinzi wa watoto na watu walioathirika katika Kanisa. Ndiyo masuala msingi katika mada ya siku kwenye Kamati ya kudumu ya Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Afrika ya Kati (Aceac), kwenye  Mkutano wao uliofanyika hivi karibuni  huko mjini Bukavu, Congo  DRC.

Na kama hiyo haitoshi pia kuendelea kwa ukatili wa virusi vya ebola, mvua nyingi katika miezi ya hivi karibuni ambayo imesababisha vifo

Wakati wa kazi yao ya mkutano kwa mujibu wa ujumbe wao wa mwisho maaskofu wamebainisha hali halisi ya sasa kijamii inayoleta wasi wasi kubwa katika nchi tatu kuanzia ukosefu wa usalama katika baadhi ya maeneo, kwa namna ya pekee katika mipaka, mahali ambapo panasalia kuwapo makundi ya mgambo ya kutumia silaha. Maaskofu pia wameonesha  kuwa kupunguza nguvu ya ununuzi ni kupunguza viwango vya maisha vya familia nyingi ambao tayari wanaishi na  umaskini. Na kama hiyo haitoshi pia kuendelea kwa ukatili wa virus vya ebola, mvua nyingi katika miezi ya hivi karibuni ambayo imesababisha vifo  hata uharibifu mkubwa wa nyumba na zana mbalimbali. Kufuatia na hili Maaskofu wa Afrika ya Kati wameweza kupongeza juhudi za Caritas na Tume ya Haki na amani mahalia, ambazo zimejikita katika kusaidia watu waliokumbwa na maafa hayo, pia  wanarudia kuwaomba wakristo wote waendelee kuonesha mshikamano kwa  waathirika hao.

Maaskofu wamepyaisha ahadi zao za kufanya kazi pamoja na madhehebu mengine ya kidini

Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Afrika ya kanda ya Maziwa makuu (Aceac)  wanatoa wito wa kuwa na dhamiri nyoofu katika srikali za Kinshasa, Gitega  na Kigali na ili kuweza kuweka moyoni suala la usalama na matarajio mema ya watu. Kuzorota kwa hali ya kisiasa katika nchi hizo tatu  kiukweli kuna hatari  ya kuzidisha tishio la mapigano ya silaha ambayo yanaendelea hasa katika majimbo ya kaskazini-mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC. Kwa upande wao, maaskofu wamepyaisha ahadi zao za kufanya kazi pamoja na madhehebu mengine ya kidini kwa ajili ya  amani ya kudumu katika Kanda ya  Maziwa Makuu.

Lazima kuwepo na muundo wa kushughulikia ripoti za unyanyasaji wa kijinsia, ikionyesha mchakato mzima ambao lazima ufuatwe

Mada nyingina mabay pia ilikuwa katika mpango wa kazi yao ilikuwa ni kutazama majimbo katoliki ya Congo, Rwanda na Burundi juu ya  usimamizi na ulinzi wa watoto wadogo na watu walioathirika katika Kanisa kwa mwanga wa mwongozo wa Motu Proprio “Vos estis lux Mundi”, uliotangazwa na Papa Francisko mara baada ya Mkutabo mjini Vatican wa mwezi Februari 2019 kwa marais wa Mabaraza ya Maaskofu katoliki duniani kote. Hati hiyo ya kipapa inapendekeza kwamba kufika  Juni mwaka huu, tayari kila jimbo liwe na muundo wa kukubaliwa na kushughulikia ripoti za unyanyasaji wa kijinsia, ikionyesha mchakato mzima ambao lazima ufuatwe.

 

 

 

 

 

 

 

21 January 2020, 16:06