Tafuta

Maaskofu wanasema kuwa hata jamii ya Afrika ya kusini imebobea  tayari katika mantiki za kiulimwengu na ambazo katika kukua unaanza kuweka pembeni Kanisa na Injili,tafakari na tamaduni Maaskofu wanasema kuwa hata jamii ya Afrika ya kusini imebobea tayari katika mantiki za kiulimwengu na ambazo katika kukua unaanza kuweka pembeni Kanisa na Injili,tafakari na tamaduni  

Afrika Kusini:mpango mpya wa kichunga:jumuiya moja ya uinjilishaji katika huduma ya Mungu!

Katika hitimisho la Mkutano Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Afrika Kusini,wametoa Mpango Mpya wa Kichungaji unaohusu Jumuiya moja ya Uinjilishaji kwa ajili ya huduma ya Mungu, ya ubinadamu na kazi ya uumbaji wote.Na hii ni kusasisha mpango huo uliokuwapo tangu 1989.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Kubadilisha nanma ya kuwa nini  Kanisa leo hii Afrika ya Kusini ili iweze kutangaza Injili kwa namna ya kweli na uhai zaidi katika mantiki ya mwendelezo wa utamaduni na kijamii. Ndiyo lengo la mpango wa Kichungaji wa Baraza la Maaskofu nchini Afrika Kusini, katika  kutaka Jumuiya ya kuinjilisha kwa huduma ya Mungu, ya ubinadamu na kazi yote ya uumbaji. Matunda hayo ni karibu ya miaka 10 ya kutafakari ambayo yamo katika Hati iliyotolewa rasmi tarehe 26 Januari 2020  huko Soweto mara baada ya Mkutano wao mkuu wa maaskofu wa Sacbc, unaounganisha maaskofu 29 wa Afrika  Kusini kuanzia Botswana na  Eswatiti (ex Swaziland).

Hati  hiyo inajibu daima zile  dharura ambazo zimejionesha kwa miaka hii ya mwisho  katika Mabaraza ya Maaskofu Afrika ya Kusini na ili kufikia kusasisha  mpango wa mwisho wa Kichungaji wa mwaka 1989 kwa mwanga wa maendeleo ya kijamii, kisiasa, na kiutamduni katika nchi za Afrika ya Kusini hasa baada ya suala la ubanguzi. Kama alivyokumbusha Mwenyekiti wa Baraza la maaskofu Sithembele Sipuka, wakati wa mchakato wao wa mkutano huko Pretoria,  kwamba “hata jamii ya Afrika ya kusini imebobea  tayari katika mantiki za kiulimwengu na ambazo katika kukua unaanza kuweka pembeni Kanisa na Injili, kwa tafakari na tamaduni, juu ya sheria na matukio mbalimbali ya kijamii”.

Changomoto  sasa  ni mbili:  Kwa mujibu wa Hati hiyo inasema kuwa , kwa upande mmoja ni kutaka kutoa  uhai  ile imani na tasaufi ya waamini huku wakiwatia moyo katika kupyaisha uhusiano wao binafsi, Kristo na jirani, na mbapo inatakiwa kuanzishwa utume mpya wa uinjilishi katika Kanisa la Afrika ya Kusini na zaidi kuwajumuisha walei ili waweze kuwa hai na chachu ya mashuhuda wa Kristo; na kijamii katika jamii ambayo leo bado inaona migogoro ya nguvu katika sera za kisiasa, na kijamii, pia ongezeko la ukosefu wa usawa  vurugu za ubaguzi, ufisadi, uhalifu na ukosefu wa usalama.

Kwa ukaribu wa mambo  hayo ni muhimu, yanayohusiana  na  ambayo yanazingatia mpango mpya wa kichungaji uliowekwa na Baraza la Maaskofu Afrika ya Kusini Sacbc ambao, alielezea Askofu  Sipuka, kwamba yanataka kusaidia Kanisa la Afrika Kusini ili kuhama kutoka katika huduma ya kichungaji iliyokuwa na  tabia ya kuhifadhi na ili kuingia katika uhai wa umisionari  kama anavyohimiza Papa Francisko katika Wosia wake wa “Evangelii Gaudium”. Hati hiyo imeundwa na kurasa 12 ya maandishi  ambayo yamegawanywa katika sehemu nane za mada zinazohusi uinjilishaji; malezi na kuhamasisha jukumu la walei; maisha na huduma ya makuhani na mashemasi; ndoa na familia; vijana, haki ya kutotumia nguvu; uponyaji na mapatano; utunzaji wa kazi ya uumbaji na mazingira.

27 January 2020, 15:58