Katika barua ya Maaskofu wa Sudan na Sudan Kusini wanawakumbusha viongozi wa kisiasa juu ya magoti ya Baba Mtakatifu akiwaomba wapeleke Amani kwa watu na nchi yao Katika barua ya Maaskofu wa Sudan na Sudan Kusini wanawakumbusha viongozi wa kisiasa juu ya magoti ya Baba Mtakatifu akiwaomba wapeleke Amani kwa watu na nchi yao 

Maaskofu Sudan wawakumbusha wanasiasa sala ya Baba Mtakatifu

Tare 11 Aprili mwaka huu wakati wa mafungo ya kiroho kwa ajili ya viongozi wa kisiasa wa Sudan ya Kusini, Baba Mtakatifu alipiga magoti na kuwabusu huku akiwaomba wapeleke amani kwa watu wao na nchi yao. Kufuatia na mgogoro unaotaka kuzuka hivi karibuni Maaskofu wa Sudan na Sudan Kusini wameandika barua kwa viongozi hao kuwakumbusha tena ishara hiyo.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Matumaini yetu ni kuwa viongozi wetu wa kisiasa katika nchi ya Sudan Kusini, serikali na vyama vya upinzani, sehemu kubwa ikiwa ni wakristo wanaweza kweli kujikita katika ya wito  na ishara maalum aliyoifanya  Baba Mtakatifu Francisko na kuwaomba wapeleke amani katika ndugu wa Sudan ya Kusini. Ni uthibitisho maneno ya  Maaskofu wa Sudan na Sudan Kusini katika ujumbe wao uliosomwa wakati wa  Misa ya tarehe 1 Novemba 2019 katika Makanisa yote ya Sudan.

Baba Mtakatifu aliwaomba viongozi wapeleke amani kwa watu 

Hata hivyo ikukbukwe kuwa tarehe 11 Aprili 2019 wakati wa kuhitimisha mafungo ya kiroho katika Nyumba ya Mtakatifu Marta (Domus Sanctae Marthae), Vatican, kwa viongozi wa kisiasa wa Sudan Kusini, Baba Mtakatifu Francisko mbele yao alitoa tamko lenye nguvu kwa ajili ya wakati endelevu wa Serikali mpya ambayo ilikuwa izaliwe  tarehe 12 Mei  kwa kutumia ishara ya kuwabusu miguuu Rais wa Jamhuri Salva Kiir Mayardit, na Makamu Rais waliokuwapo na kati yao Riek Machar na  Rebecca Nyandeng De Mabior.

Wasiwasi wa kuzuka mgogoro tena nchini Sudan Kusini

Uundaji wa serikali mpya ya umoja wa taifa lakini uliharishwa kwa  mara nyingine tena na kwa sasa unatarajiwa  tarehe 12 Novemba 2019, japokuwa Rais Salva Kiir amewezesha kufanya mafunzo ya mtendaji bila uwepo wa Riek Machar. Kama ndiyo hivyo, taarifa zinabainisah kwamba kuna wasiwasi mkubwa wa kuzuka  tena kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe, katika nchi ambayo imeshakuwa na  mgongoro mkubwa  kwa sababu ya athari za mzozo uliotokea kunako Desemba 2013, ambao unaongezewa na uharibifu uliosababishwa na mafuriko yaliyoathiri maeneo makubwa ya Sudan Kusini.

Maaskofu wa Sudan wanasema tumeona majeraha ya watu

Kufuatia na wasiwasi huo Ujumbe wa Maaskofu wa Sudan Kusini wanathibitisha “Tumeona majeraha na majonzi ya watu wetu katika kambi za watu waliohamishwa ndani katika nchi zetu mbili na katika kambi za wakimbizi katika nchi jirani. Tunahisi na kushiriki hali ngumu za kiuchumi za watu wetu huko Sudan na Sudani Kusini”. Katika Ujumbe wao uliofikia Shirika la Habari za Kimisonari Fides, Maaskofu wanasisitiza kuwa mizizi ya migogoro inapaswa ikatwe kabisha kutokana na tamaa ya kutaka mabavu na utajiri, na ambayo kwa upande wao hutumia mgawanyiko wa koo na kikabila ili kushinikiza watu kupigana kati yao. Maaskofu wanahitimisha kwa kutoa wito juu ya  umoja ili kukabiliana pamoja na shida hii ya tofauti ili kushirikishana  rasilimali chache  walizo nazo lakini kwa faida ya wote.

MAASKOFU-SUDAN KUSINI
07 November 2019, 14:37