Kenya:ameuwawa Padre Michael Maingi Kyengo
Mwili wa padre Michael Maingi Kyengo, Paroko msaidizi wa parokia ya Thatha, jimbo Katoliki la Machakos nchini Kenya aliyekuwa ametekwa nyara tangu tarehe 8 Oktoba amekutwa amezikwa karibu na mto wa Mashamba huko Makima, karibu na Embu. Habari kutoka katika Shirika la Habari za kimisionari Fides zinasema Padre Kyengo, mwenye umri wa miaka 43 alionekana mara ya mwisho tarehe 8 Oktoba. Na tarehe 11 wanafamilia wake walikwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ya kupotea kwake.
Hata hivyo kuhusiana na upelelezi zaidi umefanywa na kugunduliwa mshukiwa kutokana na kushikwa kwa simu ya mkono, gari na kadi ya Benki ya padre huyo aliyekuwa amepotea. Baada ya kumweka mbaloni huyo mtu, amewapeleka polisi hadi mahali mbapo wamekuta mwili wa Padre Kyengo. Upelelezi huo unabainisha kwamba muuaji huyo alimkaba kwanza na baadaye akamkata koo. Kijana huyo aliyekamatwa ni Michael Muthini Mutunga, mwenye umri wa miaka 25 na ambaye wanasema hakuwa peke yake bali na watu wengine ambao kwa sasa wanatafutwa! Padre Kyengo alikuwa amepewa daraja la Upadre kunako mwaka 2012 na tangu wakati huo alikuwa anatoa huduma ya kikuhani katika parokia ya Thatha nchini Kenya.