Bado siku chache Papa Francisko atembelee kisiwa cha Madagascar
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Ni katika Wiki ya kufunga kijumuiya, ambayo ni uzoefu wa sala ya kimya na kushirikishana Injili kila mwaka ambapo watu wengi hukusanyika katika mji utwao wa Vijana huko Cuneo katika moyo wa Chama cha Kitume cha Charles de Foucauld ambapo ni maelfu ya watu hasa ushiriki wa vijana wengi. Katika wingi huo mwandishi wa Vatican News alikutana watawa watatu wanaofahamu Madagascar vizuri na mmoja ni Sr. Lucia akiwa ameadhimisha hivi karibuni miaka 60 ya maisha ya kitawa aliyekuwa na macho ya kimcheza cheza sana kwa furaha hasa ya kukumbuka miaka 25 ya utume wake alioufanya kisiwani Madagascar.
Watu wa Madagascar ni wakarimu wanamsubiri Papa kwa hamu
Sr. Lucia katika mahojiano amethibitisha juu ya kutambua vema kipindi hiki cha watu kumsubiri Baba Mtakatifu Francisko katika ziara yake ya kitume, ambapo amaesema kwa hakika itakuwa ni sikukuu kubwa!. Watu wa madagascar ni wakarimu na wenye moyo mzuri. Sr. Lucia anakumbuka alipokuwa huko akitoa huduma katika meza ya watoto wadogo, na watoto walitokea kumpenda kwa namna ya pekee. Walikuwa wakimkumbatia kwa nguvu zote. Amesema kwamba walimfundisha mambo mengi na anahisi kupokea mengi sana kutoka kwao kuliko yeye aliyweza kutoa kwao. Hadi sasa amesema, kuhisi ile shauku ya kurudi katikati ya umati wa watu hao watakao kuwa wanampokea Baba Mtakatifu kisiwani Madagascar.
Lala ni sista kutoka Madagascar, anatoa ushuhuda wa watu wake rahisi
Naye Sr. Lala ni kijana mtawa kutoka Madagascar, ambaye anajivunia nchi yake pia . Yeye ni mmoja wa idadi ya madada wa chama hicho cha kitume kilichoundwa na padre Gasparino, lakini kwa sasa anaendelea kutoa huduma karibu na wamisionari wa Italia. Akielezea nchi yake anasema “Kwa hakika katika umaskini wake, watu hawa tayari wana vinasaba na karama zao, yaani asili ya kushirikishana katika umasikini kwa upando. Anaelezea asili yake ni kutoka katika familia yenye rasilimali chache, lakini yenye kuwa na furaha ya kuishi maisha rahisi katika jumuiya nzima za vijijini. Na matumaini yake kwamba ziara ta Baba Mtakatifu Francisko inaweza kuwapelekea watu wake matumaini, katika maisha ya kila siku na katika jitihada za kanisa. Hasa vijana na Kanisa lao huko Madagascar, kisiwa ambacho kwa dhati kimeundwa na vijana wanahitaji nguvu itokayo kwa Mungu tu amsema.
Maisha ya kutengwa, kufungwa na ukoma
Misheni zao huko Madagascar zilizaliwa huko Anatihazo, moja ya vitongoji masikini zaidi katika mji mkuu. Hiyo ilikuwa miaka ya ukoloni wa Ufaransa. Kati ya wakazi katika makazi duni, katika maeneo yanayokosa kila huduma muhimu na watoto wengi bila kwenda shule , ndipo kulizaliwa shuule ndogo ya watoto wadogo na kituo kidogo cha kutoa msaada wa chakula. Wamisionari hawa ni wenye mfano mwema kwani si kwamba wanaleta miundo mipya lakini zaidi ni zawadi ya sala ya pamoja, ya kuabudu, ya ukaribu katika roho ya urafiki. Waliendelea pia hata kufungua nyumba ya Betania katika mkondo wa nchi ya Msumbiji kunako 2002, ili kushuhudia upendo wa Mungu unaoambatana na ukuaji wa kibinadamu na kiroho kwa watoto na vijana wote.