Tafuta

Maaskofu katoliki nchini Benin wanathibititisha kuendelea na mchakato wa upatanisho kati ya wapinzani wa kura ya rais nchini humo Maaskofu katoliki nchini Benin wanathibititisha kuendelea na mchakato wa upatanisho kati ya wapinzani wa kura ya rais nchini humo 

BENIN:Upatanisho wa Kanisa unaendelea kati ya mzozo wa kisiasa nchini!

Maaskofu nchini Benin wanakunusha kuhusiana na habari ya kusimamisha shughuli yao ya upatanisho wa Kanisa katika mzozo wa kisiasa,kufuatia na uchaguzi uliopingwa wa Aprili 28.Hayo yamo katika barua iliyotolewa na ofisi ya habari ya Baraza la Maaskofu kwamba haijaondoa zoezi lake la upatanisho na mazungumzo yanaendelea mara kwa mara.

Na Sr Angela Rwezaula –Vatican News

Kanisa katoliki nchini Benin halijasita kamwe kuendelea  na mchakato wa shughuli yake ya kichungaji ya kuwa kama daraja la upatanisho kati ya Serikali na nguvu za upinzani ili kutatua kipeo kigumu cha kisiasa hasa kilichotokea mara baada ya uchaguzi wa viongozi watalawala kunako tarehe 28 Aprili mwaka huu. Huo ndiyo uthibitisho kutoka  katika ofisi ya habari ya Baraza la Maaskofu nchini humo wakikanusha juu ya  habari zilizosambazwa na baadhi ta vyombo vya habari nchini humo ya kwamba Kanisa limejiondoa katika shughuli hiyo ya upatanisho.

Uchaguzi ulipingwa kutokana na kuondoa baadhi ya vyama vya kisiasa

Maaskofu walikuwa wametoa uwezekano wao wa kuingilia kati baada ya ghasia za upinzani dhidi ya  matokeo ya kura ambayo yalikuwa yamewekwa kusimamiwa na washiriki wa vya viwili tu vilivyo kuwa karibu na Rais Patrice Talon, Chama cha maendeleo na kile cha umma. Kuondolewa kwa nguvu nyingine za kisiasa, zilizo amuliwa na Tume ya uchaguzi kitaifa (Cena), ilionesha msimamo wa kukataliwa kwa nguvu kwa wapiga kura, kama ishara ya maandamano. Ni asilimia 22.99 tu ya wapiga kura waliweza kwenda kupiga kura, ambayo ilikuwa ni ya  chini kabisa katika historia ya uchaguzi nchini humo. Na tangu 1990, wapiga kura walikuwa hawajawahi kushuka kufikia chini ya asilimia 50%.

Mwezi mei ghasia zilishutumiwa na maaskofu

Mei Mosi na siku iliyofuata huko Cotonou vyama vingine vya nchi vilionyesha mapigano makali kati ya vyombo vya nguvu za serikali na mamia ya waandamanaji , tofauti ambao walikuwa wanamuunga mkono Rais mng’atuka Thomas Boni Yayi.  Ghasia hizo kwa hakika Baraza la Maaskofu katoliki walikuwa wameshutumu vikali na  kuwashauri wanasiasa waweza kufunganama kama uzi  mzito wa majadiliano ya kweli katika kulinda amani ya kijamii, umoja wa kitaifa na dhamani ya maendeleo ya usawa na upatanishi wa nchi.  

Jitihada za maskofu katika mchakato wa upatanisho kijamii nchini Benin

Katika taarifa iliyotolewa kwa siku hizi maaskofu wanathibitisha tena jitihada  zao za ya kuendelea na kwao na mchakato wa kufanya kazi kwa ajili ya upatanisho na  mshikamano wa kijamii huko Benin na wanakumbuka kuwa wamewashauri tena wakristo kusali  na kutumaini wakati wa hija ya kitaifa ya kwenda katika madhabahu ya Dassa-Zoumé iliyomalizika Jumapili 18 Agosti 2019!

23 August 2019, 15:40