Tafuta

Sinodi ya Maaskofu wa Kigiriki-Melkiti huko Lebanon wamehitimisha sinodi yao kwa kutoa azimio la kujifunza na kusambaza kwa waamini walei na mashule Hati ya Abu Dhabi Sinodi ya Maaskofu wa Kigiriki-Melkiti huko Lebanon wamehitimisha sinodi yao kwa kutoa azimio la kujifunza na kusambaza kwa waamini walei na mashule Hati ya Abu Dhabi 

Kanisa la Kimelkiti nchini Lebanon la sambazwa Hati ya Abu Dhabi

Sinodi ya Maaskofu wa Kigiriki-Melkiti huko Lebanon mara baada ya Mkutano Mkuu wao,wametoa azimio la kusambaza Hati ya Abu Dhabi kwa waamini walei,katika mashule ili kujifunza zaidi kizazi hiki na endelevu maana yake na mapadre waitumie hati hiyo katika mahubiri yao ya kawaida.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Kanisa Katoliki la Kigiriki-Melkita  nchini Lebanoni wanajiandaa kutoa nafasi kubwa ya mpango wa kichungaji hasa katika kutafakari kwa kina juu ya Hati ya udugu kibinadamu kwa ajili ya amani duniani na kuishi kwa pamoja, iliyotiwa sahihi tarehe 4 Februari 2019 huko Abu Dhabu na Baba Mtakatifu Francisko na Sheikh Ahmed al Tayyeb, Imam mkuu wa Al Azhar. Hayo yote yamethibitishwa  na msemaji wa Sinodi ya Maaskofu wa Kigiriki-Melkiti  walio unganika katika Mkutano wao mkuu hivi karibuni katika makao makuu ya Upatriaki wa Ain Traz, nchini Lebanon, chini ya usimamizi wa Patriaki Youssef Absi.

Mafunzo ya   utafiti katika shule za Upatriaki

Katika maelezo ya msemaji wa Sindo hii amefafanua juu ya lengo  azimio hili kwamba ni kutaka kuhamasaisha uelezwa zaidi katika makuzi ya kizazi kipya na endelevu kwa namna ya kuweza kijenga namna bora ya kuishi katikati ya jamii tofauti na kidini katika nchi mahali ambamo kuna hata Kanisa la Kimelkiti na mara nyingi panatokea hupotoshwaji na migogoro ya kidini na uharibifu wa kitikadi. Mpango  wa maaskofu wa kimelkiti kwa mujibu wa msemaji kuhusu Sinodi hiyo unakita kwa dhati katika masuala ya kweli  yakijuishwa iwe katika shughuli za elimu, hata zile za kichungaji. Hati juu ya udugu kibinadamu, itakuwa ni nyeti kwa mafunzo na utafiti katika shule za upatriaki na katika taasisi za kitaalimungu, wanathibitisha.

Maandiko ya Hati yatasambazwa kwa walei na mashuleni

Pia maandiko ya Hati hiyo yatasambazwa sana kati ya waamini walei  na yaliyomo ndani ya hati yaweze kutafakariwa jwa kina katika mikutano ya majimbo na maparokia. Hata mapadre wanahimizwa kujua vema yaliyomo na malengo ya Hati hiyo ya Abu Dhambi ili waweze kuyatumia wakati wa mahubiri yao ya kawaida. Wakati wa  Sinodi yao, maaskofu 24 wa upatriaki waliokuwapo wamegusia pia suala la jinsi ya kulinda watoto waathirika kwa manyanyaso kwa kwa kupitia ushauri wa  Barua ya Kitume ya Baba Mtakatifu Francisko ya Vos estis lux mundi, iliyotangazwa tarehe 7 Mei 2019.

Maandalizi ya Kongamano la kiliturujia 2022 mjini Roma

Zaidi ya hayo Maaskofu  wamezindua kamati ya maandalizi ambayo itasaidi kushiriki na kutoa mchango wa Kanisa la Kimelkiti katika Kongamo kimataifa kuhusu maisha ya liturujia katika Makanisa Katoliki  ya Mashariki, inayotarajiwa kufanyika mjini Roma kuanzia tarehe 18-20 Februari 2022. Tukio hili litafanyika wakati wa fursa ya maadhimisho ya miaka 25  tangu kutolewa maagizo ya matumizi ya kanuni za Sheria ya Liturujia ya  Makanisa ya Mashariki, iliyochapishwa na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makanisa ya Mashariki kunako mwezi Januari 1996.

25 June 2019, 13:59