Ivory Coast:Kuna hofu kubwa inayotawala katikati ya watu!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Katika hitimisho la Mkutano wa 113 wa Baraza la Maaskofu nchini Ivory Coast uliofanyika huko Agboville hivi karibunu wanaandika kwamba lazima kutambua kuwa katika wakati wa kukaribia uchaguzi wa rais 2020, katikati ya watu kumejaa kutanawaliwa na hofu kwa watu. Kilio chao Maaskofu kwa ajili ya wazalendo wao ni kwamba hawataki kuona vita tena! Maaskofu wanaandikiwa kwamba hii ni hali halisi inayotokana na migogoro ya ndani ya jumuiya, matatizo ya ukosefu wa usalama, umiliki wa ardhi, kuvamia kwa misitu bila idhini, uchimbaji wa madini, kama dhahabu usio halali na matatizo yanayohusu utambulisho wa Watu wa Ivory Coast.
Ukaribu wa familia zenye matatizo
Maaskofu wakiwageukia waamini waowanadhibitisha, kwamba wako pamoja nao karibu ili kuomba kutona na upweke walio nao katika siku hizi za mwisho, na wanataka kwa pamoja kuharibu mapepo ya kizamani ya chuki na mgawanyiko. Katika maono hayo maaskofu pia wanaonesha ukaribu wa kiroho na huruma kwa ajili ya familia ambazo zimepoteza wapendwa wao na mali zao. Na wanawaomba hata wadau wpte wa kutetea maisha ya kijamii –kisiasa ili kuweza kuzuia vita isitokee.
Kufanya kila njia ya ili kuwa na amani
Baada ya makumi miaka katika kipeo kigumu cha kiuchumi nchini humo na ambacho kimesababisha majanga mabaya katika historia ya Ivory Coast na baadhi ya miezi inayoelekea kufikia mwaka 2020, maaskofu wanasema wahusika na ambao wanafikiri ni wenye madaraka, kwa ngazi zote wanaweze kufanya kila njia iwezekanavyo ili kuwa na mchakato wa mapatano ya kijamii kwa namna ya kuweza kuzuia kipeo kingine kisitokee wakati huo huo kuweza kuimarisha amani.
Kufikia mwisho wa mchakato wa kusitisha silaha
Wakigeukia serikali, Maaskofu wakuu na maaskofu wa Ivory Coast wanawaomba serikali kuendelea na kukamilisha mchakato wa kusitisha silaha kwa sababu silaha zinaendelea kuzunguka nchini humo na wasema hiyo siyo siri kwa mtu yeyote yule. Wanahitimisha wakiomba kusitishwa kwa silaha za aina yoyote ile zinazo zunguka nchini humo na kwa jina la haki ya maisha wanaomba waepuke vita kwa mara nyingine tena!