Kiasi kikubwa cha tani za taka za kielektroniki  hutoka duniani kote kuingia Barani Afrika kila mwaka kama vile viyoyozi,simu za mkono, kompyuta na mashine nyinginezo Kiasi kikubwa cha tani za taka za kielektroniki hutoka duniani kote kuingia Barani Afrika kila mwaka kama vile viyoyozi,simu za mkono, kompyuta na mashine nyinginezo 

Ghana:Kanisa linataka kuunganisha mazingira na ajira kwa vijana!

Kanisa nchini Ghana limefanya warsha hivi karibuni inayohusu kuunganisha mazingira na ajira kwa vijana kama Mradi wa Kanisa kwa usimamizi wa taka za elektroniki.Ni njia moja wapo y kutoa jibu kuhusu Wosia wa Baba Mtakatifu wa Laudato Si

Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Tatizo kubwa zaidi linalotishia ushirikiano wa kijamii, utawala wa kidemokrasia na usalama wa taifa nchini Ghana na katika sehemu nyingi za dunia ni ukosefu wa ajira wa vijana. Ni uthibitisho wa Askofu Mkuu  Philip Naameh, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la  Tamale, nchini Ghana wakati wa  kutoa hotuba katika Warsha la  Usimamizi wa mazingira, ambao ni  mpango  mkubwa wa usimamizi wa Jimbo Kuu la Ghana ambalo kwa kiasi kikubwa wanataka kuthibiti takataka za kielektroniki ambazo anasema kuwa  hutoka duniani kote kuingia Barani Afrika kila mwaka.

Kwa kuonesha hatari  hiyo kubwa Askofu Mkuu Naameh anathibtisha kwamba, kuna zaidi ya   tani 215,000  ambamo kati ya tani hizi ni ni viyoyozi vya hewa, friji, televisheni, mashine za kuosha, kompyuta, mashine ya kupuliza taka, simu za mkononi na balbu za mwanga, ambazo sehemu  nyingi hutokea bara la Ulaya. Lengo  kuanzisha  mpango huu ni kutaka  kubadili maafa ya mazingira katika fursa za ya kazi kwa vijana wa Ghana. Kwa mujibu wa Askofu Mkuu Naameh kwamba, kama ukusanyaji na uangalizi wa taka za umeme ungekuwa umepangiliwa vizuri, ungeweza kuunda nafasi za kazi kwa vijana.

Kadhalika Askofu Mkuu amesisitiza kuwa, Kanisa linataka kupitisha mbinu ya ubunifu juu ya suala hilo kwa kujifunza kuunganisha mifano ya biashara katika usimamizi wa taka za elektroniki. Katika suala hili, amekazia kuwa Kanisa linajaribu kutafuta ushirikiano ambao hutoa mtaji wa uwekezaji katika  mpango wa biashara,ambao  haujihusishi na faida bali kujihusisha zaidi katika uendelevu.

Naye Samweli Zan Akologo, mkurugenzi mtendaji wa Caritas nchini Ghana amethibitsha kuwa kuwa warsha hiyo inaonyesha mwanzo wa upanuzi wa mradi wa Kuthibiti Taka wa Caritas zaidi ya mji mkuu, wa Accra, na kuongeza kuwa hautaangalia tu juu ya  hukusanyaji wa taka za umeme, lakini pia kuunda sehemu ya kuwezesha mvunjo vunjo wa taka hizo ambao unaweza kutoa fursa ya nafasi za ajira kwa vijana. Mradi huo wa Caritas ulianzishwa mnamo Oktoba 2017, katika kujibu au kuenzi Wosia wa Baba Mtakatifu Francisko wa Laudato Si.

19 March 2019, 15:20