Tafuta

Vijana wa Kanda ya Afrika ya Kusini,baada ya uzoefu wa Sinodi ya Maaskofu kuhusu vijana na siku ya vijana Panama sasa wanataka kufanya Siku ya vijana kikanda Vijana wa Kanda ya Afrika ya Kusini,baada ya uzoefu wa Sinodi ya Maaskofu kuhusu vijana na siku ya vijana Panama sasa wanataka kufanya Siku ya vijana kikanda  

Afrika Kusini:Tafakari ya vijana kuhusu Sinodi na ombi la siku ya vijana kikanda!

Mkutano wa vijana kutoka nchi saba za Kanda ya Afrika ya Kusini ulifanyika kuanzia tarehe 5-8 Machi,ulioandaliwa na IMBISA ambao umejikita kujadili maelekezo na ushauri wa hati ya mwisho ya Sinodi ya Maaskofu kuhusu vijana iliyofanyika Oktoba Roma.Hatimaye vijana hao wanapendekeza wawe na Siku ya vijana Kikanda kwa ajili ya utume wa Kanisa

Na Sr. Angela Rwezaula-Vatican

Vijana waliowakilisha nchi saba za Afrika ya kusini wameunganika kwa pamoja ili kutafakari juu ya hitimisho la Sinodi ya Maaskofu iliyofanyika mwezi Oktoba 2018 iliyokuwa inahusu vijana, imani na manga’muzi ya miito. Na zaidi  vijana waliweza kupata maelekezo ya dhati na ushauri kuhusu Mabaraza ya Maaskofu kwa sababu Sinodi inajikamilisha yenyewe katika jumuiya zao na katika Kanda nzima ya Afrika ya Kusini, kama ilivyo hata katika mabara mengine ya dunia baada ya Sinodi ya maaskofu mjini Roma.

Kushirikishana imani

Mkutano huo ulifanyika kuanzia tarehe 5-8 Machi 2019  kwa kuandaliwa na Kanda ya Baraza la Maaskofu wa Afrika ya Kusini (IMBISA) ambapo uliwaunganisha  vijana kutoka Lesotho, Namibia, Musumbiji, Botswana, Swaziland, Afrika ya Kusini na  Zimbabwe. Aliyeongoza shughuli hiyo ni Mike Greef mjumbe wa Chama cha Maristi. Katika majadiliano, yao ndipo ilijitokeza kuona njaa ya vijana ambao wanapenda kuwasiliana kati yao; wazo la kuu la kuweza kufanya siku ya vijana kikanda ambayo inafanana na ile ya duniani.Vile vile katika kujadiliana imewawezesha kila mmoja kutoa mchango ambao kwa pamoja wameonelea kuwa ni fursa ya kutengeneza jukwa la kushirikishana imani katika Kanda hiyo.

Vijana ni cheche za matumaini

Naye Askofu Sephamola Mopeli, OMI wa Qasha's Neck nchini  Lesotho,  ambaye ni mhusika wa Kitengo cha Kichungaji cha IMBISA amefuatilia majadiliano yao yote na hata meza za mduara. Mwisho wa wa mkutano wao  aliemelezea shauku ya  vijana katika  Sinodi imeweza kuwa cheche za kweli za matumaini katika jumuia zote wanamoishi vijana. Vilevile ameonesha furaha yake ya kuona vijana wakatoliki na wenye akili wanayo ari kubwa ya kutaka kuendeleza shughuli na utume wa Kanisa.

Mikutano iliyotangulia

Hata hivyo IMBISA mwezi Julai mwaka jana, ilikuwa imeandaa Mkutano kabla ya Sinodi  kwa ajili ya maaskofu, mapadre na vijana. Na zaidi baadhi ya vijana waliudhuria katika mkutano wa maandalizi kabla ya Sinodi uliofanyika mjini Roma mwezi Machi 2018 na ule ulioandaliwa na IMBISA na vijana wengine walikuwapo katika Sinodi mjini Roma, hata Siku ya Vijana Panama. Kutokana na ushuhuda huo  wapo vijana ambao kwa sasa ni wenye uzoefu wa utume wa Kanisa na ambapo yapo matumaini kuwa nguvu hizi na shauku zinaweza kuwasaidia na kuwa mwafaka wa kupelekea mbele utume wa Kanisa endelevu. Vijana pia wameongozwa na tafakari kupitia Wosia wa Laudato si, ili waweze kuwa  msitari wa mbele wa kutunza mazingira ambamo ni nyumba yetu ya pamoja.

22 March 2019, 16:00