Tveit(Wcc):Ukarimu wa makaribisho unaweza kuokoa maisha!
Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Kukaribisha ni mtindo wa upendo ulio mkubwa na ambao hautambuliwi. Anaadika Katibu Mkuu wa Baraza Makanisa duniani mchungaji Olav Tveit (Wcc) katika ujumbe aliowaelekeza washiriki wa Mkutano wa vijana Ulaya ulioandaliwa na Jumuiya ya kiekuemene Taize Mkutano uliofunguliwa tarehe 28 Desemba jijini Madrid nchini Uhispania unaoongozwa na mada,“Usisahau makaribisho”.
Jumuiya ya taize inawakilisha vema maana ya uekumene
Makaribisho siyo suala la fadhila iliyomo ndani mwetu tu, bali hata yanaingia katika mahusiano ya kukaribisha, kupokeana na kujenga urafiki wa kweli na wa kuaminiana wakati wa kushirikishana chakula na malazi. Makaribisho ni hatua muhimu sana na lakini pia iliyo na hatari wakati mwingine, anaandika mchungaji Tveit, ambapo anafikiri kuwa, kukaribisha pia ni karama maalum ya jumuiya ya kiekumene ya Taize, jumuia ambayo inawakilisha vema nini maana ya chama hicho cha Uekumene.
Tunageuka kuwa nyumba yetu hapa duniani kwa mwaliko wa Mungu
Kukaribisha wengine katika nyumba zetu ina maana ya kuwaalika katika mioyo yetu. Anaendelea kuandika mchungaji Tveit na kwamba pia ni wito msingi katika Biblia na ni sura yenyewe na uwepo wa Mungu kwa maana Mungu ni nyumba yetu, haijalishi tunamoishi au tunakwenda wapi kwa maana sisi wenyewe tunageuka kuwa nyumba ya Mungu hapa duniani.
Upendo huo wa kukaribishana ambao tumepewa bure na kwa namna ya unyenyekevu, unahitajika sana katika nyakati zetu leo hii. Anasema hayo akiwakumbuka wahamiaji na wakimbizi, wasio kuwa na makazi na wenye kuhitaji, hata ambao kiurahisi ni tofauti na sisi. Makaribisho yetu mema yanaweza kuokoa maisha, kuunda jumuiya, hata kuokoa wakati wetu. Kwa maana hiyo Mchungaji Tveit kwa vijana waliokusanyika Madrid anawapa angalisho la kuwa makini kwa chama hiki cha Kiekumene kwa maana ni chama cha upendo na si tu kwa wakati ujao bali kuanzia hata sasa.
Bila uzoefu wa kukutana haiwezekani kujenga Ulaya
Wakati huo huo naye Askofu Mkuu wa Madrid Kardinali Carlos Osoro akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa vijana amesema: “uzoefu wa kidugu, kugundua mwingine kuwa ni ndugu, kwa sababu Mungu yupo ndani mwake na mwangu na anatupenda, ndiyo ujumbe muhimu wakati huu kwa vijana wakristo wa Ulaya. Na huo ndiyo ujumbe ambao Bara la kizamani la Ulaya linataka kuwaleza vijana wote wa Ulaya wanaoudhuria mkutano huo, ulioandaliwa na Jumuiya ya Kiekumene ya Taize katika mji uliojengwa na watu wote wanaotoka nchini Uhispania na sasa kutoka dunia nzima!
Kardinali ambaye pia ni mdau wa mikutano hii, kwani katika miaka ya 60 hata yeye mwenye alikuwa anakwenda katika jumuiya ya Taize Ufaransa. Kwa maana hiyo anathibitisha kuwa, kuna umuhimu wa mkutano huo kwa sababu ya ukimya na kusikiliza. Hivi ni viungo viwili ambavyo vikikosekana, huwezi kumpata Mungu na wala ndugu. Ni hali ambayo inamsaidia mtu kukutana na kuingia binafsi kwa ukina wa moyo wa kujitafiti wewe ni nani na ni kitu gani tunafikiria. Kwa kufanya hivyo ndipo inazaliwa hata sala ya Baba Yetu, inayotufundisha kushikamana na ndugu kama anavyotukambatia Mungu Baba. Kardinali Osoro anasema bila uzoefu huo haiwezekani kujenga Ulaya, na bila kufanya hivyo watagawanyika kila mmoja katika eneo lake na mipaka yake, bila kuwa na madaraja ambayo Bwana anaomba kila mmoja ajenge, kwa utambuzi kuwa kila kaka na dada ni ndugu kuanzia jinsi anavyofikiri. Na iwapo itafikia hatua hiyo ya udugu ni hakika kuwa dunia utabadilika.