Sudan Kusini:Maaskofu wanaendelea kusali kwa ajili ya amani!
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Afrika ya Mashariki (AMECEA) pamoja na Serikali za Ethiopia na Kenya, Uganda na Sudan wametoa mchango wa pamoja katika kufikia hatua ya kutia sahini ya makubaliano ya amani kati ya Sudan na viongozi wapinzani. Kwa sasa inabidi kusali ili amani iweze kudumu, kwa mujibu wa Askofu Erkolan Lodu Tombe, wa jimbo la Yei akiwaalika wote kuanzia walei na macleri wote waendelee kusali bila kuchoka.
Tuendelee kusali ili kusitisha umwagaji damu na kujenga amani ya kudumu
Tunahitaji kusali na ni matumaini ya kwamba sala zinawezeka kusitisha umwagaji wa damu na kuunda amani ya kudumu kwa watu ambao wanateseka huko Sudan Kusini, anathibitisha Askofu katika vyombo vya habari za kimisionari Fides. Kwa mujibu wa Askofu Tombe, anasema, baada ya kutia sahini ya makubaliano ya amani kati ya serikali na viongozi wa upinzani iliyotiwa mwezi Agosti mwaka huu, hali kwa kiasi chake kuna utulivu sehemu nyingi za nchi na hiyo imewajaza imani na matumaini kwa watu wengi, lakini hata hivyo Askofu PIA anabainisha kuwa bado kuna hali ambayo siyo nzuri ya wanamgambo ambao hawakutia sahini katika makubaliano hayo.
Katika baadhi ya maeneo, mara nyingi makubaliano hayo yanakiukwa na vurugu zinaendelea: lakini hiyo ni matukio ambayo yanaweza kutokae katika baadhi ya sehemu zote duniani. Ni lazima kukubali kwamba hakuna makubaliano ambayo ni makamilifu. Licha ya hayo yote, Askofu Tombe anaonesha juu ya imani yake kwamba vita na vurugu vinaweza kusistishwa kabisa na kutoa fursa ya watu ili waweze kujenga maisha yao.
Viongozi kuomba ruhusa kwa maandishi ya kukutana na wanamgambo wapinzani
Pamoja na viongozi wengine wa dini wa Yei, Maaskofu wa AMECEA wamomba ruhusa ya kwa mandishi kwa upand ewa Serikali wa kuwaruhusu wao waende kukutana na wanamgambo ambao bado wanakataa mkataba huo na ili kuweza kuwahusisha katika mazungumzo na kuwasikiliza hoja zao na mara baada ya mazungumzo wataweza kueleza serikali na watu wake. Hadi sasa lakini bado hawajapata ruhus hiyo, kwa maana wao waliwajibu kuwa wako huru kwenda, lakini jambo hili kwa upande wa viongozi wa dini haikuwa inatosha. Maana wanahitaji uthibitisho wa maandishi, ni kwa njia hiyo tu, inaweza kuwahakikishia usalama kwa yule ambaye atajikita katika utume huo wa mazungumzo ya amani, amehitimisha Askofu Tombe.