Kardinali Berhaneyesus amekutana na Waziri Mkuu wa Hungaria  akiwa nchini  Ethiopia Kardinali Berhaneyesus amekutana na Waziri Mkuu wa Hungaria akiwa nchini Ethiopia 

Ethiopia:Vijana wasaidiwe kupata elimu na fursa za ajira ili wabaki nchini mwao!

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya nchi ya Hungaria Daktari Tristian Azbej wakati wa ziara yake nchini Ethiopia mapema wiki iliyopita,amekutana na Kardinali Berhaneyesus, CM Askofu Mkuu wa Addis Ababa na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Ethiopia (CBEC)

Sr. Angela Rwezaula- Vatican

Katika mkutano kati ya Waziri wa  Mkuu wa Jamhuri ya Hungari na Kardinali Berhaneyesus Souraphiel, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Addis Ababa nchini  Ethiopia amesema kuwa taifa la Ethiopia linakabiliwa na shida za  uhamiaji na usafirishaji wa binadamu  na kwa kutumia njia mbadala ya kupata suluhisho inawezekana  kupitia elimu ya vijana. Amethibitisha hayo, mwishoni mwa wiki iliyopita alipokutana na waziri huyo, akiwa katika ziara nchini Huko. Kardinali anasema kuwa Kanisa Katoliki Ethiopia linajitahidi kukabiliana na shida ya uhamiaji kwa kutafuta  fursa mbalimbali  za nafasi ya ajira kwa vijana iliwaweze kunufaika na kujenga taifa lao.

Unyanyaswaji kwa wahamiaji ni picha mbaya sana

Akiendelea kusisitiza umuhimu wa kuelimisha vijana,  Kardinali  Berhaneyesus amefafanua kuwa wakati vijana wanapohama  wanakabiliwa na hatari ya kifo na kwa wale ambao wanajaliwa kufika  mwisho wa safari wanakabiliwa na hatari ya unyanyaswaji na  kwa upande huo, anamesema inasikitisha sana na siyo picha nzuri ya kutazama. Kwa hivyo amependekeza vijana kubaki katika nchi yao ili waweze kuiboresha na kwa wale ambao wangependelea kupata riziki mahali penginepo basi, waweze kutayarishwa kuhusu vikwazo na hatari wanazoweza kukabiliana nazo.

Akizungumzuia juu ya madhara wanayoyapata wahamiaji, Kardinali amethibitisha kwamba  hii ni shida kubwa nyingine ambayo inawakabili wahamiaji wakati wanapofika mwisho wa safari yao na  ambayo huwafanya kukata tamaa baada ya kutambua kuwa  hali ya maisha ni kinyume na matarajio yao. Kutokana na hiyo, anasisitiza kuwa elimu ni kigezo muhimu  cha kuweza kupata mwafaka wa vijana hao katika maisha na ili waweze kubaki mahalia, japokuwa matatizo ya uchumi na ukosefu wa ajira bado unaikumba nchi ya Ethiopia.

Elimu kwa vijana ni ufunguo dhidi ya kuhama nchi mahalia

Kadhalika Askofu Mkuu wa Ethiopia akijikita kuelezea juu ya kupata elimu kwa vijana, kutokana na kwamba, vijana waliohitimu elimu ya kutosha , ni kiegezo muhimu katika taifa na kwa manufaa yao. Hata hivyo amweze kuwapongeza  kuwepo kwa vijana wengi nchini Ethiopia ambao wamepata wafadhali wa masomo kutoka nchi ya Hungaria na baada ya kufuzi masomo yao wamezea kurudi mwakwao na ili kusaidia  uboreshaji wa nchi!

Kwa upande wake Waziri  Azbej ya  nchini ya Hungaria amesema ni furaha kubwa kwake kutambua kuwa vijana ambao wamepokea ufadhili wa masomo katika nchi ya Hungaria wamerejea katika nchi yao na wanasaidia katika kuendeleza na  kuboresha nchi. Kadhalika amesema kuwa nchi yake imejitolea kuwasaidia wakristo ambao wanaoteswa duniani na kwa njia ya pekee anasifu ushirikiano baina  ya Kanisa Katoliki la Ethiopia na nchi ya Hungaria katika tendo la kuwafikia watu maskini. Mwisho Waziri Azbej amemwalika Kardinali Berhaneyesus na viongozi wote wa kidini kutembelea nchi ya Hungaria!

 

10 December 2018, 14:29