A.Kusini:Lazima kuhusisha wanawake na vijana zaidi katika kazi!
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Matatizo ya ajira nchini Afrika ya kusini ndiyo yanakabiliwa uso kwa uso na vijana, na kwa maana hiyo, “Tunayo matarajio makubwa kutoka kwa wanawake vijana wasio kuwa na ajira kuwa wawakilishi wazuri katika mpango mzima unatafuta namna ya suala hili la kipeo cha ajira. Na hatuwezi kuzungumza juu yao bila kuwa nao. Ni vema kuwahusisha wanawake na vijana zaidi”. Haya yamethibitishwa na Askofu Abel Gabuza, Askofu wa Jimbo la Kimberly na Rais wa Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu wa Afrika ya Kusini. Ni katika ujumbe wake alioutoa kwa rais, Bwana Cyril Ramaphosa wa Afrika ya Kusini ili kuhakikisha kunakuwepo mchanganyiko wa uwakilishi wa kazi kwa upande wa wanawake na vijana katika Jukwaa kuhusu kazi, Jukwaa linalitarajiwa kufanyika mwaka kesho 2019.
Pongezi ya kupyaisha mipango mipya
Licha ya maombi hayo pia Askofu Gabuza ameonesha furaha yake, “ kwa ajili ya uongozi wake rais hasa kuhusiana na chachu ya sasa ya kutaka kupyaisha mipango, pamoja na maamuzi yake ya kuimarisha mipango mipya ya uwekezaji. Askofu Gabuza anamwalika Rais kupitia chama chake tawala ambacho kinaonesha hatima ya maendeleo ya taifa ambayo bado hayajawa ya kweli, kwa maana hiyo ni mtarajio yao wanaweza, “kuongoza vema katika matokeo ya usimamizi unao hitaji kutekelezwa katika hali halisi ya uchumi.
Idadi ya watu wa Afrika Kusini inakabiliwa na hali mbaya ya uchumi, kuongezeka kwa bei ya vitu vya msingi, na kuongezeka kwa ukosefu wa ajira. Mashirika mengine ya kiraia yameomba hata ruzuku ya kipato cha msingi na kutazama kwa upya juu ya misaada wa mshahara kwa vijana. Amehitimisha Askofu Gabuza akisema: “Tunatarajia kuwa rais na baraza lake la mawaziri watatafakari kwa makini mapendekezo hayo”.
Matarajio ya serikali kuongeza idadi ya watu walio ajiriwa, kutoka kwa milioni 11 hadi milioni 24
Mkutano wa mwaka huu wa kazi ulifanyika tarehe 4 na 5 Oktoba 2018. Kulingana na Rais Ramaphosa, mipango na makubaliano ya ajira wamekubaliana na washiriki kuundwa kwa ajira 275,000 kwa mwaka. Takwimu juu ya ajira nchini Afrika Kusini zinaoneesha kuwa, pamoja na ukuaji wa ajira ya nafasi 206,000 katika robo ya pili ya 2018, lakini bado kuna kiwango cha ukosefu wa ajira wenye 27.2%. Kwa mujibu wa mpango wa kitaifa wa maendeleo, serikali inatarajia kuongeza idadi ya watu walioajiriwa, kutoka kwa milioni 11 hadi milioni 24 kufikia mwaka 2030.