Tafuta

Uchungu wa Kanisa la Pennsylvania sababu ya manyanyaso ya watoto na watu wazima waathirika Uchungu wa Kanisa la Pennsylvania sababu ya manyanyaso ya watoto na watu wazima waathirika 

Ni aibu kubwa na majuto kutokana na nyanyaso kwa watoto!

Maswali ya kina na uchungu mkubwa yametokana na nyanyaso ambazo Kanisa linakosa hata sehemu ya kijiweka kwa maana ni aibu. Ndiyo maelezo ya Maaskofu Katoliki wa Serikali ya Pennsylvania nchini Marekani wakati wa kujibu ripoti iliyotolewa kuhusu nyanyaso iliyowakilishwa mapema Jumanne wiki hii kwa umma.

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Katika majibu ya maaskofu  katoliki wa serikali ya Pennsylvania katika Majimbo ya Filadelfia  wanaandika kuwa, ni uchungu  kwa kila anayesoma , kwa namna ya pekee wale ambao waliathirika na manyanyaso ya kijinsia na kwa familia zao. Wanasitikika kwa kina kwa  uchungu wao na kwamba wabaki katika nia ya uponywaji. Askofu wa Pittsburgh ameandika tamko lake kuwa hakuna sababu yoyote ambayo inataka kupunguza kile kilichotujia, Wote kwa pamoja majibo nane ya Serikali ya Pennyslvania wamejibu  kwa mujibu wa ripoti  iliyo anandaliwa na wanasheria wakuu, raimu walio pewa kwa mujibu wa haki za machakato wa Marekani katuka mchakato ambao haukuwa wazi na kwa msaada wa polis ili kufanya uchunguzi juu ya uwezekano wa mantendo haya ya kihalifu. Uchgunzo ulikuwa wazi kwa mkuu wa uchunguzi wa Serikali.  Walichunguzia majimbo 6 ya Pennsylvania , wakati majimbo mengine mawili yalikuwa tayari yamekwisha anza uchunguzi huo.

Zaidi ya waathirika 1000.

Imechukua miaka miwili kwa mahakimu kukamilisha ripoti yenye kurasa 900. Na hiyo inahusu manyanyaso yaliyotokea katika serikali ya Pennsylvania na kutendwa na wahusika wa Kanisa Katoliki. Ripoti inatazama miaka 70  ya mwisho na kuwezesha kuendesha mchakato kimpangilio,na  hata kama hakuna kesi mpya zilizogunduliwa, lakini mepatikana waathirika 1000 japokuwa wanasema namba hiyo inawezekana kuwa kubwa kwa ujumla. Ripoti hiyo ni kamili zaidi ambayo haikuwahi kutolewa na taasisi za Serikali ya Marekani juu ya kesi za  manyanyaao. Zaidi ya majina yaliyotajwa katika ripoti, inajitokeza  sehemu kubwa ni wahusika wa Kanisa, na janga zaidi ni kutokana na kufunika kesi hizo.

Hakuna mwenye kosa nalindwa.

Ni lazima kupambana na uhalifu huo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hakuna tena mtoto kuathirika na wale watenda kosa wanafichwa, Jimbo la Scranton linathibitisha! Katika mtandao wa jimbo hilo, kuna hata majina 70 ya wenye  makosa ambao ni mapadre, walei na wangine ambao wametajwa katika ripoti na wanasheria wakuu . Jimbo laErie linataja watu 34 na  maeneo wanayoishi pia wanataja haya majina 31 ambao wameshakuwa marehemu. Kati ya majina 65 kuna mwanamke mmoja na askofu mmoja. Kwa mujibu wa Mtandao wa jimbo. Askofu   kwa namna ya pekee hakufuatilia na kuchunguza juu ya  mashtaka ya manyanyaso katika jimbo lake alilokabidhiwa. Askofu wa Jimbo la Erie mons. Lawrence Persico amewaandikia moja kwa moja waathirika wa manyanyaso hayo.

Sala na usimamizi.

Katika majimbo yote kama inavyoelezea ripoti yenyewa, inasisitiza kuwa miaka ya mwisho, hasa kwa miaka kumi, kumekuwapo na maendeleo makubwa kwa jinsi ya uwazi uliojionesha. Hii ndiyo njia ya kufuata, kwa mujibu wa wachunguzi na wapelelezi. “Tutendelea kufanya malipizi kwa dhambi zetu za wakati uliopita na kusali wakati huo huo kuwa na usimamizi  kwa ajili ya waathirika wa matendo haya”, anasisitiza Askofu Ronald W. Gainer wa Jimbo la Harrisburg, na kuongeza kusema, tutajitahidi kufuata na kuhakikisha kunakuwapo mabadiliko chanya ili kuhakikisha kwamba majanga haya harudiwi tena…. Ninaka watoto, wazazi, wanaparokia, wanafunzi , watu wote , makleri na umma watambue kuwa makanisa yetu na mashule ni yenye uhakika; kutakuwa na uwajibikaji mkubwa wa kulinda kila yoyote atakayeingia kupitia milango yetu”.

17 August 2018, 15:43