Tafuta

Raha ya milele uumpe ee Bwana Askofu msaafu  Nestori Timanywa, na Mwanga wa Milele Umwangazie, apumzike kwa amani Amina Raha ya milele uumpe ee Bwana Askofu msaafu Nestori Timanywa, na Mwanga wa Milele Umwangazie, apumzike kwa amani Amina 

Askofu mstaafu Timanywa wa Jimbo Katoliki Bukoba ameaga dunia!

Taarifa iliyotolewa na Mhashamu Baba Askofu Deusderius Rwoma wa Jimbo Katoliki la Bukoba Tanzania imeeleza kuwa, Baba Askofu Mstaafu Nestori Timanywa amefariki dunia kwa ugonjwa wa saratani majira ya saa tano asubuhi ya tarehe 28 Agosti 2018

Sr. Angela Rwezula - Vatican

Askofu Mstaafu wa Jimbo Katoliki la  Bukoba  Mhashamu Nestori  Timanywa alifariki dunia tarehe 28 Agosti 2018 , katika Hospitali ya Rufaa Bugando, Mwanza  alikokuwa amelazwa kwa matibabu. Misa ya mazishi itafanyika tarehe 31 Agosti 2018 katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Bikira Maria Mama mwenye Huruma Jimboni Bukoba ikitanguliwa na masifu ya jioni.

Taarifa iliyotolewa na Mhashamu Baba Askofu Deusderius Rwoma wa Jimbo Katoliki la Bukoba Tanzania imeeleza kuwa, Baba Askofu Mstaafu Nestori Timanywa amefariki dunia kwa ugonjwa wa saratani majira ya saa tano asubuhi ya tarehe 28 Agosti 2018.

Akitoa utaratibu wa mazishi ya Askofu Mstaafu Nestori Timanywa kupitia Radio MBIU, Askofu Rwoma amesema kuwa, maziko yatafanyika Ijumaa tarehe 31 Agosti kwenye Kanisa Kuu la Bikira Maria, Mama Mwenye Huruma Jimboni Bukoba, yakitanguliwa na Masifu ya Jioni.

Askofu Mstaafu Nestori Tumanywa alizaliwa tarehe 7 Mei 1937 katika Kijiji cha Kakungiri, Parokiani Mugana, baada ya majiundo yake akapewa daraja Takatifu la Upadre  tarehe 11 Desemba 1966 na Mwadhama Lauren  Kardinali Rugambwa. Kunako tarehe 26 Novemba 1973 akachaguliwa na Baba Mtakatifu wa wakati ule Papa  Paulo wa VI, kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Bukoba  na kusimikwa rasmi kunako tarehe  24 Februari 1974.

Amestaafu tangu tarehe 15 Januari 2013, akiwa na umri wa miaka 75. Na tarehe 28 Agosti 2018 akiwa na umri wa miaka 81 ameitwa kwa Mungu Baba.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake libarikiwe leo na hata Milele!

Kwa maelezo zaidi:  http://www.bukobadiocese.co.tz/bishopsofbukoba.php

30 August 2018, 16:11